LIVE STREAM ADS

Header Ads

CHAMA CHA AFYA YA JAMII CHAWAOMBA WADAU KUTOA USHIRIKIANO ILI KUPAMBANA NA MATUMIZI TUMBAKU KWA VIJANA.

Dk. Adeline l. Kimambo(kulia) kutoka Chama cha Afya ya Jamii (TPHA) akitoa muhutasari wa Madhara ya Tumbaku mbele ya waandishi wa habari pamoja na wageni waalikwa waliofika kujadili changamoto wanazokabiliwa nazo hasa wanapokuwa wanatoa huduma kwa jamii kuhusu matumizi ya Tumbaku na kuwaomba wadau hao kutoa ushirikiano wa kutosha ili kufikia malengo waliyojiwekea.Katikati ni Dk Faustine Njau kutoka Chama cha Afya ya Jamii (TPHA).
(Picha na Geofrey Adroph wa Pamoja Blog)
Mratibu wa Mradi wa Madhara ya Tumbaku (TPHA) Dk. Bertha T.A. Maegga(kushoto) akizungumza jambo kwenye kikao kilichowashirikisha wadau mbalimbali kutoka katika manispaa za jijii la Dar es Salaam kuhusu kushirikiana na wadau mbalimbali hasa kutoka katika manispaa za jiji hilo ili kudhibiti matumizi na madhara ya Tumbaku hapa nchini na kusisitiza kushirikiana ili kupambana na janga hili hapa nchini linalopelekea kupoteza nguvu kazi kubwa.
Dk. Faustine Njau kutoka Chama cha Afya ya Jamii (TPHA) akisisitiza wadau kujitokeza na kushirikiana nao ili kutatua tatizo la matumizi ya tumbaku pamoja na vileo hasa kwa watoto wadogo wanaoanza kutumia wakiwa wadogo na kupelekea kupata madhara udogoni.Ambapo kwa utafiti uliofanyika umeonesha asilimia 6 ya watoto 400 wa shule za msingi walianza kutumia tumbaku wakiwa hawajui madhara yake.
Mjumbe wa Chama cha Afya ya Jamii (TPHA),Dk. Mashombo Mkamba akizungumza jambo wakati wa majadiliano ni kwa namna gani wanaweza kupunguza matumizi ya Tumbaku katika jamii unayowazunguka na hata kuwaomba wadau mbalimbali kushirikiana ili kuongeza nguvu katika mapambano dhidi ya matumizi ya Tumbaku hasa kwa watoto wadogo ambao ni nguvu kazi ya baadae.
Dk.Tulitweni Mwinuka kutoka manispaa ya Temeke akieleza changamoto wanazozipata pale wanapokuwa wanatoa elimu ya matumizi ya Tumbaku na kusisitiza changamoto kubwa wanayoipata ni wanasiasa kutotoa ushirikiano wa kutosha kwa kuhofia kupoteza wapiga kura wao wakati wa uchaguzi.

No comments:

Powered by Blogger.