MKUMBO: UHAMISHO WA ASKARI ULIOFANYIKA MKOANI MWANZA UMELENGA KULIBORESHA JESHI.
Na:George Binagi-GB Pazzo wa Binagi Media Group
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza
Charles Mkumbo amefafanua kwamba mabadiliko ya askari wa Usalama barabarani
yaliyofanyika hivi karibu Mkoani hapa, yalikuwa ni mabadiliko yenye lengo la
kuimarisha zaidi utendaji kazi wa jeshi hilo.
Kamanda
Mkumbo alitoa ufafanuzi huo hii leo mbele ya waandishi wa habari, kufuatia
uvumi ulioenea mitaani kwamba askari hao walibadilishwa vitengo vyao vya kazi
kutokana na utovu wa maadili kazini ikiwemo kujihusisha na vitendo vya rushwa.
Amefafanua
kwamba takribani askari 78 katika Wilaya saba za Mkoa wa Mwanza, walibadilishwa
vitengo pamoja na vituo vyao vya kazi na kwamba mabadiliko kama hayo
yataendelea kufanyika ndani ya vitengo vingine vya jeshi hilo.
Mabadiliko
hayo yalihusisha Wilaya za Nyamagana, Ilemela, Kwimba, Magu, Sengerema na
Misungwi ambazo utendaji kazi wa askari hao ulikuwa ukilalamikiwa na wananchi
ambapo Wilaya ya Ukerewe haikuguswa na pangua pangua hiyo.
Katika hatua
nyingine, Kamanda Mkumbo amebainisha kuwa, mvua iliyonyesha jumatatu ya wiki
hii imesababisha kifo cha mtu mmoja pamoja na watu wengine zaidi ya 300 kukosa
makazi ya kuishi, baada ya nyumba zao kuezuliwa na upepo mkali uliokuwa
umeambatana na mvua hiyo.
Amemtaja
aliefariki dunia kuwa ni Mzee Hollo Masamwa (80) Mkazi wa Kwimba, aliefariki
dunia baada ya kuangukiwa na ukuta wa nyumba aliyokuwa akiishi.
No comments: