UMOJA WA WAENDESHA BODABODA MKOA WA MWANZA WATOA TAMKO KWA BODABODA WOTE NCHINI.
Na:George Binagi-GB Pazzo @BMG
Umoja
wa Waendesha pikipiki (Bodaboda) Mkoa wa Mwanza, umewahimiza Waendesha pikipiki
wote nchini kusherehekea kwa amani Sikukuu ya Mwaka Mpya huku wakitimiza vyema
majukumu yao kwa kufuata sheria na taratibu za Usalama barabarani.
Mwenyekiti wa Umoja huo Makoye Kayanda Bunoro
ametoa rai hiyo wakati akizungumza na BMG (Binagi Media Group), ikiwa zimesalia siku tatu kuuaga
mwaka huu wa 2015 na kuukaribisha mwaka mpya 2016.
“Niwaombe Waendesha pikipiki wote nchini
washerehekee kwa amani shamrashara za kuukaribisha mwaka mpya, kuanzia mkesha huku
wakitimiza majukumu yao kwa kuzingatia sheria za usalama barabarani na
kuondokana na fujo zisizo za lazima ikiwemo kuchoma matairi barabarani kwa
misingi ya kuukaribisha mwaka mpya 2016”. Amesema Bunoro.
Bunoro ameongeza kuwa ni vyema bodaboda wote
wakatimiza majukumu yao kwa kutii sheria bila shuruti ikiwemo kutoendesha
pikipiki huku wakiwa wametumia vilevi pamoja na kuzidisha abiria (mishkaki)
ikizingatiwa kwamba bodaboda ni kazi halali hivyo waendane na kauli mbiu ya
Mhe.rais Dkt.John Pombe Magufuli ya “Hapa Kazi Tu” katika kutimiza majukumu
yao.
Pia amewahimiza watumiaji wengine wa barabara
wakiwemo waendesha vyombo vya moto kama magari pamoja na watembea kwa miguu nao
kuzingatia sheria za usalama barabarani ili kuepukana na ajali zinazozuilika.
No comments: