LIVE STREAM ADS

Header Ads

WAFANYAKAZI WA KIWANDA CHA PEPSI JIJINI MWANZA WAGOMA.

Na:Binagi Media Group
Wafanyakazi wa Kiwanda cha Soda cha Pepsi kinachomilikiwa na Kampuni ya SBC Tanzania Jijini Mwanza, leo wamegoma kufanya kazi kiwandani hapo wakishinikiza mwajiri wao kuwaboreshea maslahi yao.

Wafanyakazi hao ambao wanafanyaka kazi kwa mkataba wa muda mfupi (vibarua), wamedai kuwa wamefikia hatua hiyo kutokana na manyanyaso wanayoyapata kutoka kwa mwajiri wao ambae ni Wakala wa ajira katika Kiwanda hicho, Kampuni ya SARAMA Investiment ambayo hata hivyo wamebainisha kuwa imefutiwa kibali cha kusimamia ajira zao kiwandandani hapo.

Wamefafanua kwamba Kampuni ya SARAMA Investment imekuwa ikisimamia ajira zao kinyume cha sheria za kazi, kwa kuwa jukumu la Kampuni hiyo kiwandani hapo lilikuwa ni kushughulikia suala la kutafuta wafanyakazi na kwamba suala la malipo linafanywa na kampuni ya SBC Tanzania tofauti na ilivyo sasa ambapo kampuni hiyo ya Uwakala wa ajira ndiyo inayoshughulikia malipo yao.

Wamesema kutokana na hali hiyo, Kampuni ya SARAMA Investment imekuwa ikiwanyima haki zao ikiwemo kuwalipa malipo kidogo ya shilingi Elfu Sita kwa Kutwa, badala ya shilingi Elfu Tisa kwa kutwa na kwamba wamekuwa wakifanya kazi kwa muda mrefu jambo ambalo wamesema hawatakubaliana nalo.

Itakumbukwa kwamba wiki chache zilizopita, Waziri wa nchi, ofisi yaWaziri Mkuu, Sera, bunge, ajira, kazi, vijana na walemavu Mhe.Jenista Muhagama, alifanya ziara katika Kiwanda hicho na kutoa maagizo ya kufuta leseni ya Kampuni inayolalamikiwa na wafanyakazi hayo ya SARAMA Investiment kwa kukiuka sheria za ajira nchini.
INSERT…………..WAFANYAKAZI

Katika ziara aliyoifanya katika kiwanda cha Pepsi Jijini Mwanza, Mhe.Muhagama aliagiza ajira za wakafanyakazi hao kusimamiwa na Kampuni inayomiliki Kiwanda hicho ambayo ni SBC Tanzania huku akitamka kufuta leseni ya Kampuni ya SARAMA Investment inayolalamikiwa ambayo bado inasimamia ajira za wafanyakazi hao.
INSERT……………JESTINA MUHAGAMA

Hadi tunakwenda katika chumba cha habari, mazungumzo ya kutatua mgomo huo yalikuwa yakiendelea baina ya wawakilishi wa wafanyakazi hao, Viongozi wa Kampuni ya SARAMA Investment pamoja na afisa ajira Mkoa wa Mwanza ambapo wanahabari hawakuruhusiwa kuingia katika mazungumzo hayo.

No comments:

Powered by Blogger.