LIVE STREAM ADS

Header Ads

NI MHIMU KUFANYA YAFUATAYO IKIWA UNAADHIMISHA SIKUKUU YA PASAKA.

Bonyeza HAPA KUSOMA Sehemu ya Kwanza.

YESU KRISTO; PASAKA YETU LEO
Katika Agano la Kale, Pasaka ilianza kwa damu ya kondoo. Lakini Yesu Kristo alikuja duniani na kujitoa Yeye kuwa Pasaka yetu badala ya kondoo kama ilivyokuwa hapo zamani katika Agano la Kale. Kwa sasa tunapoadhimisha Pasaka katika maisha yetu, damu ni muhimu sana, ila sasa siyo damu ya kondoo, bali ni Damu ya Yesu Kristo.

Yesu Kristo alitupa sisi Damu yake badala ya Damu ya kondoo. Katika Luka 22 kuanzia mstari wa 7 tuanaona namna Bwana Yesu alivyosheherekea Pasaka pamoja na wanafunzi wake, tukio ambalo ndiyo lilikuwa mwanzo kabisa wa meza ya Bwana ambayo huwa tunashiriki leo makanisani na sehemu mbalimbali.

Katika Pasaka hii, Yesu Kristo aliwapa wanafunzi wake mkate (kuashiria mwili wake) na divai (kuashiria Damu yake) na akawapa mkate na kusema “Huu ni mwili wangu unaotolewa kwa ajili yenu, fanyeni hivi kwa ukumbusho wangu” (Luka 22:19) na pia akawapa divai na kuwaambia “Kikombe hiki ni Agano Jipya katika Damu Yangu, imwagikayo kwa ajili yenu” (Luka 22:20).

Hivyo basi, tangu wakati huo wa maagizo ya Bwana Yesu, tunaadhimisha Pasaka kwa kuinywa Damu ya Yesu na kuula mwili wake kama alivyotuelekeza, na ndiyo maana huwa tunashiriki meza ya Bwana huku tukila mkate ikiwa ni kama tendo la Imani kuwa tunakula mwili wake Yesu, na kuinywa divai au mzao wowote wa mzabibi kama tendo la imani kuwa tunainywa Damu ya Yesu Kristo (Imani bila ya matendo imekufa nafsini mwake).

DAMU YA YESU
Tunapoadhimisha Pasaka,ni jambo la lazima sana kwamba uitafakari Damu ya Yesu na kuona ni kwanini Yesu aliimwaga Damu yake kwa ajili yako wewe na mimi. Damu ya Yesu ndiyo mtaji tuliopewa kwa ajili ya mafanikio yetu ya kila eneo la maisha yetu.

Yesu Kristo alimwaga Damu yake katika matukio tofauti kwa maana zake tofauti pia:
Yesu alimwaga Damu yake alipotahiriwa kama ishara ya Damu ya Yesu kuitahiri mioyo yetu, yaani kuifanya mioyo yetu kuifuata sheria ya Mungu kwa ukamilifu wake wote.

Yesu alimwaga Damu yake ilipotoka kama tone la jasho alipokuwa akiomba katika bustani ya Gethesmane ili kuvunja ile laana Mungu aliyomlaani Adamu na kumwambia kuwa “Kwa jasho la uso wako utakula chakula chako…” (Mwanzo 3:19, Luka 22:44)
Damu ya Yesu ilitoka katika kichwa chake alipovikwa taji ya miiba, Damu hii ni kwa ajili ya kukomboa namna yetu ya kufikiri/kufanya maamuzi.

Damu ya Yesu ilitoka katika mkono wake wa kushoto na kulia, Damu hii ni kwa ajili ya kuibariki na kuleta uhai katika kazi za mikono yetu.

Damu ya Yesu ilitoka katika moyo wake, Damu hii ni kwa ajili ya kuleta uzima na uponyaji katika ndoa.
Damu ya Yesu ilitoka katika miguu yake miwili, Damu hii itaifanya miguu yetu kuwa na shauku ya kwenda kutenda mema, na Damu hii inatumilikisha kila mahali ambapo nyayo za miguu yetu zitapakanyaga.

Je, ni eneo gani ambalo unataka msaada wa Mungu? Ichukue Damu ya Yesu na umwombe Mungu juu ya eneo hilo. Unaruhusiwa kunywa Damu ya Yesu, lakini pia, kwa kadiri ya imani yako, unaweza kupakaa katika sehemu yoyote ile ya mwili wako au popote ambako unataka msaada wa Damu ya Yesu.

Katika kipindi hiki cha Pasaka, acha mazoea, bali itafakari Damu ya Yesu na gharama Bwana Yesu aliyoilipa hadi hivi leo tunapata baraka kwa kuitumia Damu yake.

Soma mistari ya Biblia inayozungumzia tukio zima la kuteswa,kufa,kufufuka na kupaa kwa Yesu, pia angalia filamu/video zinazoonesha matukio haya kama vile “The Passion of the Christ” au ile filamu ya Yesu “JESUS-KISWAHILI” Hivi vitakusaidia sana kuona gharama aliyoilipa Yesu kwa ajili yako ili ujue namna Yesu Kristo anavyokupenda. Pia nenda Kanisani, na baada ya ibada pata muda wa kukaa na kutafakari habari hizi za upendo wa Yesu.

TUOMBE…
“Mungu Baba, ninakuja mbele zako kwa Damu ya Yesu Kristo. Mungu Baba, asante kwa kunipenda kwa kiasi kikubwa namna hii, maana Neno lako linasema, “Kwa maani jinsi hii Mungu uliupenda ulimwengu, hata ukamtoa Mwanao wa pekee, ili kila amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele”. Bwana Yesu, ninaamini ya kwamba Wewe ni Mwana wa Mungu, na ninaamini kwamba ulija duniani, ukateswa,ukafa na ukafufuka kwa ajili yangu.

Ninakuomba unisamehe dhambi zangu zote, na ninakukaribisha katika moyo wangu na maisha yangu yote, Wewe uwe ndani yangu na mimi niwe ndani yako, na Jina langu uliandike katika kitabu kile cha Uzima cha Mwanakondoo. Ninaomba Damu yako idhihirike katika maisha yangu na kunipa uzima ndani yako. Asante Bwana Yesu kwa kunipenda na kuniokoa, AMEN!!! Damu ya Yesu Kristo ikutunze sasa na hata milele, Amen.
Kwa Msaada wa Mtandao

No comments:

Powered by Blogger.