CHAMA CHA MAPINDUZI WILAYANI MWANGA CHAKIRI KUPITIA WAKATI MGUMU.
Kaimu Katibu Mkuu UVCCM Taifa, Shaka Hamdu Shaka
akikabidhi Kadi za chama kwa wanachama wapya baada ya kufungua Shina la Vijana Wakereketwa wajasiriamali Kilang'wa Wilayani Mwanga.
Na:Fahadi Siraji
Pamoja na kukiri kupitia siasa za majitaka wakati wa Uchaguzi Mkuu uliofanyika mwaka jana, Chama Cha Mpinduzi CCM Wilaya
ya Mwanga Mkoa kilimanjaro kimesema bado wanachama wake ni imara na wamoja na kwamba wasiokubali kuyumbishwa kisiasa.
Hayo yalisemwa jana na Katibu wa CCM Wilayani humo, Mwanaidi Hussein Misha, wakati akitoa neno la shukran mara baada
ya Kaimu katibu Mkuu UVCCM Taifa Shaka Hamdu
Shaka kuzungumza na viongozi wa vijiji, kata pamoja na wanachama wa chama hicho katika Wilaya hiyo.
"CCM iliioachwa na marehemu
baba Taifa Mwalimu Julius Nyerere, Mzee Abeid Karume, Mzee Rashid Kawawa na Mzee Thabit Kombo itabaki kuwa kimbilio na tarajio la wananchi wengi katika
kufanikisha masuala yao ikiwemo ya kisiasa, kijamii na kiuchumi. Alisema Misha na kuongeza;
"Shaka nimekuwa nikikusikiasikia
tu katika vyombo vya habari, wewe bado ni kijana mdogo ila unatosha
kubeba hata dhamana kubwa, endelea Mungu atakusaidia ili uthibitishwe kuwa Katibu Mkuu kwa kuwa uwezo unao wa kukitumikia vyema
kiti hicho" Aliongeza Mbisha.
Awali Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa
kilimanjaro, Juma Raibu Juma, aliisifu Wilaya ya Mwanga kwa kuendelea kuwatoa
mchanga wa macho kwa kulinda jimbo hilo lisichukuliwe na upinzani.
Kaimu Katibu Mkuu UVCCM Taifa, Shaka Hamdu Shaka, anaendelea na
ziara yake Mkoani Kilimanjaro na baadae ataelekea katika Mikoa ya Tanga
Wanachama wapya wakila kiapo cha Chama
Mti wa kumbukumbu mara baada ya kuwasiri katika
ofisi ya Wilaya ya Mwanga Mkoani Kilimanjaro
Katibu Mkuu UVCCM Taifa, Shaka Hamdu Shaka
akizungumza na wanachama wa CCM Mapema
Wilayani Mwanga
Kaimu Katibu Mkuu Shaka Hamdu Shaka akikabidhi
Mpira kwa kiongozi wa Timu ya soka ya vijana wa CCM Wilayani Mwanga
Kaimu Katibu Mkuu Shaka Hamdu Shaka, akikadhi Jezi kwa Captain wa Timu ya Kileo juu
Mkuu wa Utawala, Omary Mwanang'walu
akisalimia wananchi Wilayani Mwanga
Mwenyekiti UVCCM mkoa wa Kirimanjaro
Juma Raibu akizungumza katika Mkutano wa Hadhara
Kaimu Katibu Mkuu UVCCM Taifa, Shaka Hamdu Shaka
akihutubia wananchi katika mkutano wa Hadhara Wilaya ya Mwanga Mkoa wa
Kirimanjaro.
No comments: