ANUSURIKA KIFO BAADA YA KUJIRUSHA KUTOKA KWENYE MNARA WA SIMU JIJINI MWANZA.
Kijana Mmoja Jijini Mwanza amenusurika kifo baada ya kujirusha kutoka katikati ya mnara wa simu.
Na BMG
Tukio hilo limetokea hii leo na kuvuta watu wengi waliofika kumshuhudia kijana huo ambae amepanda katika mnara huo tangu majira ya asubuhi na kukatalia mnarani hadi majira ya saa sita mchana.
Mashuhuda wa tukio hilo ambao pia ni marafiki wa karibu na kijana huyo, wamesema huenda kijana huyo amefikia maamuzi hayo kutokana na ugumu wa maisha ambao amekuwa akiulalamikia huku wengine wakisema ni kutokana na kuathiriwa na matumizi ya dawa za kulevya ikiwemo gundi ambayo amekuwa akiyatumia.
Akizungumza kwa niaba ya Kamanda wa jeshi la uokoaji na zima moto mkoani Mwanza, mmoja wa maafisa wa uokoaji Mussa Kaboni, ametoa rai kwa makampuni yenye minara ya simu kuimarisha ulinzi katika minara hiyo ili kuondoa hatari inayoweza kujitokeza kutoka kwa raia wasio wema.
Baadhi ya mashuhuda wa tukio hilo walionekana kuchukizwa na kitendo cha kijana huyo na kusikika wakifoka kwa hasira na makelele ya hali ya juu "rukaa, ruka sasa, jirushe kama wewe ni mwanaume" hali ambayo ilikuwa ikimuongezea morari kijana huyo na hivyo kujirusha kweli kutoka katikati ya mnara huo.
Baada ya kijana huyo kujirusha kutoka katikati ya mnara hadi chini, alipoteza fahamu na kukimbizwa katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Mwanza, Sekour Toure kwa ajili ya huduma ya kwanza.
Zoezi la uokoaji lilichukua zaidi ya masaa sita bila mafanikio
Kijana huyo akiwa katika kilele cha mnara huo uliopo barabara ya makongoro-Airpot jijini Mwanza
Kijana akiwa hoi baada ya kujirusha kutoka katikati ya mnara
Kijana akiwahishwa hospitalini huku akiwa hoi baada ya kujirusha kutoka katikati ya mnara
Mussa Kaboni, kutoka kikosi cha uokoaji na zima moto jijini Mwanza, akizungumza na wanahabari
Mmoja wa mashuhuda akitoa maoni yake kuhusiana na tukio hilo.
Mmoja wa mashuhuda na ambae alikuwa akisaidia katika zoezi la uokoaji, akizungumzia tukio hilo.
Umati wa wakazi wa jiji la Mwanza wakishuhudia tukio la kijana huyo
Ghafla kuna jamaa mmoja akatuhumiwa kwa wizi na hapo shughuli nyingine ya kumuokoa na yeye ikaanza upya.
No comments: