LIVE STREAM ADS

Header Ads

WAUGUZI KATIKA HOSPITALI YA RUFAA BUGANDO JIJINI MWANZA WAOMBA KUTOBAGULIWA.

Jana May 13,2016 Tanzania imeungana na Mataifa mbalimbali duniani kuadhimisha "SIKU YA WAUGUZI DUNIANI" ambapo Kitaifa Maadhimisho hayo yamefanyika Mkoani Geita.
Imeandaliwa na BMG

Jijini Mwanza, Maadhimisho hayo yalifanyika katika Hospitali ya Rufaa ya Bugando ambapo huduma yaliambatana na huduma mbalimbali ikiwemo wananchi kuchagia damu.

Katika Maadhimisho hayo, Wauguzi katika Hospitali ya Rufaa Bugando Jijini Mwanza, walihimiza zaidi kuondolewa kwa matabaka yaliyopo baina yao na Watendaji wengine wa afya wakiwemo Madaktari kwa kupewa thamani sawa hususani kuboreshewa maslahi yao ikizingatiwa kwamba hakuna huduma bora ikiwa Wauguzi pamoja na Madaktari watafanya kazi bila ushirikiano.

Uongozi wa Hospitali hiyo ulikiri kwamba Wauguzi ni watu muhimu katika sekta ya afya na kwamba mahitaji yao yataendelea kuboreshwa zaidi ili kuendana na umuhimu wao. 
Kauli Mbiu; Maslahi Bora kwa Wauguzi, Vifaa Tiba vya Kutosha, Chachu ya Kutoa Huduma Bora kwa Wagonjwa/Wateja.
Baadhi wa Wauguzi kutoka Hospitali ya Rufaa Bugando wakiwa katika Maadhimisho ya Siku ya Manesi Duniani, ambapo waliiomba Hospitali hiyo kuondoa matabaka miongoni mwao na madaktari hususani kuboreshewa maslahi yao ikiwemo malipo ya muda wa ziada kazini kama ilivyo kwa Madaktari.
Baadhi wa Wauguzi kutoka Hospitali ya Rufaa Bugando wakiwa katika Maadhimisho ya Siku ya Manesi Duniani, ambapo waliiomba Hospitali hiyo kuondoa matabaka miongoni mwao na madaktari hususani kuboreshewa maslahi yao ikiwemo malipo ya muda wa ziada kazini kama ilivyo kwa Madaktari.

No comments:

Powered by Blogger.