LIVE STREAM ADS

Header Ads

FASTJET YATANGAZA FURSA NYNGINE KWA WATEJA WAKE.


Dar es Salaam 30 Mei 2016 – Fastjet, shirika la ndege la bei nafuu Afrika  limezifanya ndoto za usafiri  kuwa za kweli  kwa abiria wake zaidi ya milioni mbili  waliopaa anga za Afrika tangu kuzinduliwa kwake Novemba 2012.

Ukiwa kama mkakati wa kuhamasisha hata Watanzania wengi zaidi  kusafiri, fastjet  imetangaza kwamba abiria yeyote anayenunua tiketi  kuanzia Jumanne Mei 31 ataingia kwenye  bahati na nasibu  ya kwanza ya aina yake  ijumulikanayo Big 10 draw ambapo washindi 10 watasafiri bure   katika njia yoyote  ya fastjet katika mtandao wake barani Afrika.

Kwa watu kumi watakaoshinda bahati nasibu hiyo  shirika linawapa uwezo wa kwenda katika mapumziko  au kwenda katika safari ya manunuzi  pamoja na marafiki  na familia  jambo wamekuwa wakiliwazia  kila mara.

Ama kwa wajasiriamali wa Tanzania, safari hiyo inaweza kutumia kukuza mahitaji ya biashara kwa kuokoa  gharama za usafiri katika safari nyingine kumi wanazozihitaji  kusafiri.

“Ni rahisi, lengo la fastjet ni kufanya uwezekano kwa wateja wengi kusafiri, iwe ni kwa shughuli za biashara, kutembelea marafiki  na familia, au kufurahia burudani ya kusafiri,” alisema Meneja Mkuu wa fastjet Tanzania John Corse.


 Njia ambazo zinahusiana  kwa ajili hiyo ni safari za kutoka Dare es Salaam kwenda Mbeya, Mwanza, Kilimanjaro, Zanzibar, Nairobi, Entebbe, Lusaka, Harare na Johannesburg hali kadhalika safari  kati ya Kilimanjaro na Harare.

Tiketi zitakazonunuliwa Jumanne Mei 31, 20016 kwa njia za kimataifa na  za ndani  zitawawezesha abiria wake kuingia katika bahati nasibu ya Big 10. Washindi watatangazwa Juni 2016 na safari 10 za bure  ni lazima zifanyike  kabla ya Desemba 11, 2016.

Ikitambuliwa kama shirika la ndege la gharama nafuu Afrika, fastjet hivi sasa inafanya safari  ndani ya nchi 11 kwa wafanyabiashara, watali na familia ambazo zimeipokea tozo lake la nauli nafuu na linalofikia kwa usafiri wa anga.

“Usafiri wa anga ni ufunguo unaoendelea kuhamasisha na kukuza uchumi wa Tanzania  kwa kuufanya uwe rahisi kwa familia, wafanya biashara  na watalii kumudu kusafiri,” alisema Corse  na kuongeza, “tumezindua punguzo hili la nauli  hivyo kwamba hata wasafiri wanaweza kuzoea usafiri wa anga wanaoumudu, iwe wanasafiri kwa ajili ya biashara au mapumziko.”

Kukata tiketi kiunaweza kufanyika kwa njia ya mtandao kupitia www.fastjet.com, kupitia wakala aliyethibitishwa au kwa kuwasiliana na na fastjet kupitia +255 784 108 900. Malipo pia yanaweza kufanyika kwa fedha taslimu, kwa njia ya mtandao kwa kutumia kadi au  malipo kwa njia ya mitandao ya simu.

No comments:

Powered by Blogger.