LIVE STREAM ADS

Header Ads

UTALII WA NDANI WAZIDI KUPATA MASHIKO.

Nyumbu akiwa amepumzika mara baada ya kula nyasi.
Na Dickson Mulashani

Suala la utalii wa ndani limeonekana kupata mashiko baada ya wanafunzi wa chuo kikuu cha Stefano Moshi Memorial University College (SMMUCo) kuhamasika na kuamua kutembelea hifadhi ya taifa ya Ngorongoro ili kujionea vivutio vya kipekee vinavyopatikana katika mbuga hiyo.


Akizungumzia safari hiyo mmoja wa wanafunzi hao, Emmanuel Kalenzi, amesema waliguswa kupanga ziara hiyo kuunga mkono wadau mbali mbali wanaohamasisha utalii wa ndani ili kuweza kuwa mabalozi kwa wengine. “Sisi kama wasomi ndio tunapaswa kuwa mabalozi kwa jamii inayotuzunguka na ili uwe balozi mzuri basi uwe umashajionea kwa macho”  alisema.

Ndege aina ya Cranes nao wanapatikana katika eneo la crater


Nyati dume mwenye umri mkubwa ambaye tayari ametengwa na kundi lake 


Simba dume  akiwa anaunguruma.
Simba jike akiwa amepumzika kwenye nyasi 
Wanafunzi wakiwa katika geti la kuingia hifadhi ya Ngoro ngoro.
Picha zaidi Bonyeza HAPA

No comments:

Powered by Blogger.