MSAJILI WA VYAMA VYA SIASA NCHINI ATAKA MWAFAKA DHIDI YA ZUIO LA MAANDAMANO NA MIKUTANO YA KISIASA.
Ikiwa Una Habari, Tukio, Picha, Maoni au Tangazo, Wasiliana Na BMG Kwa Nambari za Simu 0757 432694 Au Email binagimediagroup@gmail.com
Na James Salvatotory
Msajili wa vyama vya siasa nchini, Jaji Francis Mutungi, amevitaka vyama ambavyo vinampango wa kuandamana na kufanya mikutano ya hadhara, kutokufanyaka hivyo na badala yake vikae katika meza ya mazungumzuko ili kutafuta mwafaka wa zuio la mikutano na maandamano nchini.
Akizungumza jana na waandishi wa habari Jijini dar es salaam, Mutungi alisema kwenye Taifa lolote lile kama kuna kuwa na sintofahamu, njia sahihi ya kuitatua ni mazungumzo na kuwaomba wadau wenye mpango wa mikutano na maadamano wasubiri kwanza na watumie mazungumzo kuleta mwafaka.
Aidha Jaji Mutungi aliwatoa hofu wananchi kuhusu taharuki ya uvunjifu wa amani ambayo imejengeka miongoni mwao kutokana na kauli za maandamano zilizotangazwa na wanasiasa nchini.
No comments: