MAMA WA MITINDO ASYA PAMOJA NA MASTAA WA BONGO KUPAMBA JUKWAA LA "PLUS SIZE FASHION SHOW" ZANZIBAR.
Ikiwa Una Habari, Tukio, Picha, Maoni au Tangazo, Wasiliana Na BMG Kwa Nambari za Simu 0757 432694 Au Email binagimediagroup@gmail.com

Mama wa mitindo maarufu kama Asya Idarous Khamsin ataonesha mitindo yake kama mgeni mwalikwa kwenye "Plus Size Fashion Show" inayo tegemea kufanyika huko Zanzibar Jumamosi ya Tarehe 8 August 2016 katika Hotel ya Grand Palace.
Asya amejipatia Shavu hili,kupitia kampuni ya mitindo ya Zanzibar inayo tambulika kama "Style House" chini ya C.E.O Mama Titi ambaye anaishi uingereza.
Ingawa Asya anaishi Marekani lakini kwa sasa yupo hapaTanzania kwa ajili ya onesho hilo lenye dhumuni kubwa la kuchangia "Breast Cancer Zanzibar".
Mbali na Mama wa mitindindo, designers wengine pia watashiriki kikamilifu kwenye ufanisi Onesho hilo.
Special Apperance atakuwa ni mwigizaji Wastara Sajuki, Burudani itatolewa na Khadja Kopa. (Nyote mnakaribishwa).
No comments: