MWANZA WATAKIWA KUCHANGIA DAMU KWA WINGI.
Ikiwa Una Habari, Tukio, Picha, Maoni au Tangazo, Wasiliana Na BMG Kwa Nambari za Simu 0757 432694 Au Email binagimediagroup@gmail.com
Judith Ferdinand, Mwanza
Wananchi mkoani Mwanza wametakiwa kujitolea kuchangia damu, ili kuweza kuokoa maisha ya mama mjamzito na mtoto ambao wamekuwa wakipoteza maisha kwa ukosefu wa damu.
Hayo yalisemwa jana na ofisa Uhamasishaji wa Kitengo cha Damu Salama kanda ya Ziwa Bernadino Medaa, alipokuwa akizungumza na gazeti hili.
Medaa alisema, ili kuweza kuokoa maisha ya mama mjamzito na mtoto, ni vema wananchi wawe na utaratibu wa kuchangia damu katika hospitali mbalimbali zilizopo mkoani hapa.
Pia alisema, wanawake wengi ndio wanakabiliwa na uhitaji wa damu hasa wajawazito wakati na baada ya kujifungua sambanba na watoto , hivyo ni vema kila mwananchi kujitolea ili kuweza kuokoa maisha ya wahitaji wa huduma hiyo.
Aliongeza kuwa,kila mwananchi anatakiwa kuchangia damu kwa hiyari, itakayosaidia kuokoa maisha ya mgonjwa ambaye anahitaji huduma hiyo.
"Jamii inatakiwa itambue umuhimu wa kutoa damu kwa hiyari ili kuweza kuoko maisha ya mgonjwa, kwani wenzetu wa nchi nyingine wanajitahidi kuchangia kwa wingi, ili kuondoa tatizo la ukosefu wa damu kwenye hospitali na kunusulu maisha ya mgonjwa,"alisema Medaa.
Aidha aliiomba serikali kushirikiana na kitengo hicho,kuhamasisha kuelimisha jamii kuhusu umuhimu wa uchangiaji damu salama kwani mwitikio ni hafifu.
Judith Ferdinand, Mwanza
Wananchi mkoani Mwanza wametakiwa kujitolea kuchangia damu, ili kuweza kuokoa maisha ya mama mjamzito na mtoto ambao wamekuwa wakipoteza maisha kwa ukosefu wa damu.
Hayo yalisemwa jana na ofisa Uhamasishaji wa Kitengo cha Damu Salama kanda ya Ziwa Bernadino Medaa, alipokuwa akizungumza na gazeti hili.
Medaa alisema, ili kuweza kuokoa maisha ya mama mjamzito na mtoto, ni vema wananchi wawe na utaratibu wa kuchangia damu katika hospitali mbalimbali zilizopo mkoani hapa.
Pia alisema, wanawake wengi ndio wanakabiliwa na uhitaji wa damu hasa wajawazito wakati na baada ya kujifungua sambanba na watoto , hivyo ni vema kila mwananchi kujitolea ili kuweza kuokoa maisha ya wahitaji wa huduma hiyo.
Aliongeza kuwa,kila mwananchi anatakiwa kuchangia damu kwa hiyari, itakayosaidia kuokoa maisha ya mgonjwa ambaye anahitaji huduma hiyo.
"Jamii inatakiwa itambue umuhimu wa kutoa damu kwa hiyari ili kuweza kuoko maisha ya mgonjwa, kwani wenzetu wa nchi nyingine wanajitahidi kuchangia kwa wingi, ili kuondoa tatizo la ukosefu wa damu kwenye hospitali na kunusulu maisha ya mgonjwa,"alisema Medaa.
Aidha aliiomba serikali kushirikiana na kitengo hicho,kuhamasisha kuelimisha jamii kuhusu umuhimu wa uchangiaji damu salama kwani mwitikio ni hafifu.
No comments: