LIVE STREAM ADS

Header Ads

VIJANA NCHINI WANAPENDA KUJIAJIRI KULIKO KUAJIRIWA.

Ikiwa Una Habari, Tukio, Picha, Maoni au Tangazo, Wasiliana Na BMG Kwa Nambari za Simu 0757 432694 Au Email binagimediagroup@gmail.com

Na James Salvatory, BMG Dar
Imeelezwa kuwa asilimia 50 ya vijana wanapenda kuanzisha biashara zao ikilinganishwa na asilimia 25 ambao wangependa kuajiriwa kwenye taaluma zao kama vile uhandisi, uanasheria, udaktari na ualimu

Akizungumza jana Jijini Dar es salaam katika uzinduzi wa  ripoti ya utafiti wa vijana Tanzania, Mkurugezi wa Taasisi ya  Afrika  Mashariki ya Chuo Kikuu cha Aga Khan, Alex Awet, alisema ripoti iliyohusisha vijana 1900 kutoka nchi za Kenya, Uganda, Rwanda na Tanzania inaonyesha matokeo ambayo yanaleta matumaini na wasiwasi na haja ya kuchukua hatua za haraka kwani baadhi ya matokeo ni kinyume na hali halisi inayofaa kuwepo .

“Katika mahojiano tuliofanya ni asilimia 20 tu ya vijana ambao walisema wangependa kuwa wakulima  huku walipoulizwa kuhusu wanachotathimini sana asilimia 75 walitathimini imani katika dini kwanza,asilimia 61 walitathimini kazi kwanza na asilimia 46 walitathimini familia kwanza;

Inasikitisha kuwa 75 ya vijana wa tanzania waogopa kudai haki zao kwa kuchelea adhabu  huku takiribani asilimia 45 wanaamini ufisadi una manufaa wakati asilimia 58 wanaamini kuwa haijarishi nini vip mtu atatajirika kwa njia zozote zile halali au halamu ,’’ alisema mkurugenzi huyo

Naibu Waziri ofisi ya Waziri Mkuu, sera, bunge, kazi, vijana, ajira na walemavu, Abdallah possi, alisitushwa  na asilimia 44 ya vijana ambao utafiti umebainisha wanaweza kupokea au kutoa rushwa.

“Utafiti unaonyesha asilimia 75 wanaweza kuathiri au kujihusisha na udaganyifu wakati wa kupiga kura  huku ikiwa wazi kabisa asilimia 39 walisema wangempigia kura mgombea aliyewahonga jambo ambalo siyo zuri na tunatakiwa kukipinga kwa nguvu zote na kuwaomba vijana kutambua umuhimu wa kulipa kodi kwani utafiti unaonyesha asilimia 34 pekee ya vijana wanaamini kwa dhati kuwa ni muhimu kulipa ushuru,’’ alisema posi.

No comments:

Powered by Blogger.