WASANII MKOANI MWANZA WATAKIWA KUSAIDIA UTOKOMEZAJI WA UKATILI WA WATOTO MAJUMBANI.
Ikiwa Una Habari, Tukio, Picha, Maoni au Tangazo, Wasiliana Na BMG Kwa Nambari za Simu 0757 432694 Au Email binagimediagroup@gmail.com
Judith Ferdinand, Mwanza
Wasanii mbalimbali mkoani Mwanza wakiwemo wa maigizo na muziki wametakiwa kutunga nyimbo na filami zenye kuelimisha jamii juu ya kupinga ukatili wa watoto majumbani pamoja na kutetea haki za watoto hao.
Hayo yalisemwa juzi kwenye mafunzo ya kupinga ukatili majumbani na Ofisa Uelimishaji wa Shirika lisilo la kiserikali linalojishughulisha na kupinga ukatili majumbani Foundation Karibu Tanzania (FKT)Erick Karongo,yaliyofanyika kwenye uwanja wa shirika hilo,lililopo wilayani Ilemela mkoani hapa.
Alisema kila msanii anatakiwa kukemea vitendo hivyo kupitia kazi zao za sanaa, ikiwemo nyimbo,maigizo,shairi na ngonjera za kuelimisha jamii dhidi ya ukatili
Pia alisema, lazima mzazi atambue umuhimu wa mtoto kwa kumthamini na kumpenda kwani kufanya hivyo kutapunguza ukatili kwa watoto.
Naye Mkurugenzi kikundi cha Hangano Cultulral Troupe, Peter Haule, alisema, kupitia mafunzo hayo wataelimisha jamii kwa njia ya sanaa ili kupinga ukatili kwa watoto.
“Tunalishukuru shirika hili kwa kutoa mafunzo haya, kwani tukiwa kwenye matamasha tutatunga nyimbo za kuelimisha jamii juu ya ukatili wa watoto majumbani kwani kumfanyia vitendo hivyo ni kumnyima haki yake na kinyume na sheria," alisema Haule.
Kwa upande wa Ofisa Uhusiano Johanes Emmanuel,alisema kuvunja ukimya kutasaidia kupunguza watoto wa mitaani kwani lengo la kuanzisha kituo hicho ni kutetea watoto wanaofanyiwa vitendo vya kikatili.
Judith Ferdinand, Mwanza
Wasanii mbalimbali mkoani Mwanza wakiwemo wa maigizo na muziki wametakiwa kutunga nyimbo na filami zenye kuelimisha jamii juu ya kupinga ukatili wa watoto majumbani pamoja na kutetea haki za watoto hao.
Hayo yalisemwa juzi kwenye mafunzo ya kupinga ukatili majumbani na Ofisa Uelimishaji wa Shirika lisilo la kiserikali linalojishughulisha na kupinga ukatili majumbani Foundation Karibu Tanzania (FKT)Erick Karongo,yaliyofanyika kwenye uwanja wa shirika hilo,lililopo wilayani Ilemela mkoani hapa.
Alisema kila msanii anatakiwa kukemea vitendo hivyo kupitia kazi zao za sanaa, ikiwemo nyimbo,maigizo,shairi na ngonjera za kuelimisha jamii dhidi ya ukatili
Pia alisema, lazima mzazi atambue umuhimu wa mtoto kwa kumthamini na kumpenda kwani kufanya hivyo kutapunguza ukatili kwa watoto.
Naye Mkurugenzi kikundi cha Hangano Cultulral Troupe, Peter Haule, alisema, kupitia mafunzo hayo wataelimisha jamii kwa njia ya sanaa ili kupinga ukatili kwa watoto.
“Tunalishukuru shirika hili kwa kutoa mafunzo haya, kwani tukiwa kwenye matamasha tutatunga nyimbo za kuelimisha jamii juu ya ukatili wa watoto majumbani kwani kumfanyia vitendo hivyo ni kumnyima haki yake na kinyume na sheria," alisema Haule.
Kwa upande wa Ofisa Uhusiano Johanes Emmanuel,alisema kuvunja ukimya kutasaidia kupunguza watoto wa mitaani kwani lengo la kuanzisha kituo hicho ni kutetea watoto wanaofanyiwa vitendo vya kikatili.
No comments: