LIVE STREAM ADS

Header Ads

MENEJA WA UWANJA WA CCM KIRUMBA AHIMIZA USAFI UWANJANI HAPO.

Ikiwa Una Habari, Tukio, Picha, Maoni au Tangazo, Wasiliana Na BMG Kwa Nambari za Simu 0757 432694 Au Email binagimediagroup@gmail.com

Meneja wa Uwanja wa CCM Kirumba Steven Shija (kushoto) akipokea mifuko ya saruji kutoka kwa Mwenyekiti wa Umoja wa Mafundi Mzunguko wa Uwanja huo, Michael Omollo (kulia).

Judith Ferdinand, Mwanza
Meneja  wa Uwanja wa CCM Kirumba   uliopo  wilayani Ilemela jijini Mwanza Steven Shija, amewataka wajasiriamali na mafundi wanaofanya shughuli zao, kwenye maeneo yanayozunguka uwanja huo kufanya usafi ili kuweka mazingira katika hali ya usafi ili kuepukana na magonjwa ya milipuko.

Hayo aliyasema juzi wakati alipokuwa akipokea msadaa wa  mifuko ya saruji 35  yenye thamani   ya sh 542,500 kutoka kwa wajasiriamali na  Mafundi wa mzunguko wa uwanja huo alisema,  ili kuweza kufanya kazi kwa amani  na salama bila kuugua ni vema  kila mtu akafanya usafi katika eneo lake ya kazi.

Shija alisema, ifike  wakati kila mtu atambue kuwa  tunza mazingira ya kutunze kwani  afya yako ndiyo mtaji wako kuzingatia hayo  hakuta kuwa na mtu ambaye  atafanya shughuli za kujiingizia kipato katika eneo uchafu. 

“Nawaomba  ndugu zangu mzingatie usafi, ili  kuepuka kuugua magonjwa ya mlipuko nimewaruhusu kufanyia hapa kazi nikiwa na lengo kila mtu ajipaitie kipato halali kulingana na kazi zenu,”alisema Shija.

Pia alisema,ni vema kutumia jumamosi ya mwisho ya mwezi iliyotengwa na Raise John Magufuli kama siku ya usafi, kusafisha mazingira yao ili kuwavutia na wateja wao.

Aliwashukuru wajasiliamali hao kwa kujitoa  katika kuchangia ujenzi wa miundombinu ya kupitisha maji taka kwa kutoa mifuko ya saruji 35, kwa kufanya hivyo kutasaidia  kumalizika kwa  ujenzi huo, sambamba na kuhimiza kutrunza mazingira ya eneo hilo  ili kuweza kufanya shughuli zao kwa  amani. 

Naye Mwenyekiti wa  Umoja wa Mafundi wa Mzunguko wa Uwanja wa CCM Kirumba Michael Omollo alisema,   kwa kuwa yeye ni kiongozi wa umoja huo ni jukumu lake kuhimiza kufanya usafi  katika maeneo ya kazi kwani uchafu adui.

“Tunamshukuru kiongozi huyu kwa kutukumbusha kufanya usafi  katika maeneo yetu  ya kazi, kwani kila binadamu husahau  hivyo kukumbushana ni sehemu ya kazi,”alisema Omollo.

No comments:

Powered by Blogger.