LIVE STREAM ADS

Header Ads

MKUU WA WILAYA YA MUHEZA ATEMBELEA KITUO CHA AFYA UBWARI KUJIONEA UPASUAJI WA MACHO.

Ikiwa Una Habari, Tukio, Picha, Maoni au Tangazo, Wasiliana Na BMG Kwa Nambari za Simu 0757 432694 Au Email binagimediagroup@gmail.com

Mkuu wa wilaya ya Muheza Mkoani Tanga, Hajat Mhandisi Mwanasha Tumbo katika jana akiingia kwenye kituo cha Afya Cha Ubwari, alipokwenda kuangalia zoezi la upasuaji wa macho kwa wakazi wa wilaya hiyo wanaokabiliwa na matatizo mbalimbali ikiwemo ya mtoto wa Jicho iliyoendeshwa na Taasisi ya Medewell Charitable Health Centre kulia ni Mganga Mkuu wa wilaya hiyo,Mathew Mganga na kushoto ni Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo,Luiza Mlelwa.
 Baadhi ya wazee waliofanyiwa upasuaji wakisubiri zoezi la kupatiwa dawa na miwani
 Baadhi ya wananchi waliofanyiwa upasuaji wakisubiri zoezi la kupatiwa dawa na miwani
 Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Muheza,Luiza Mlelwa akizungumza wakati wa zoezi hilo la upasuaji
 MKUU wa wilaya ya Muheza Mkoani Tanga,Hajat Mhandisi Mwanasha Tumbo akizungumza wakati wa zoezi la upasuaji huo.
 MKUU wa wilaya ya Muheza Mkoani Tanga,Hajat Mhandisi Mwanasha Tumbo wa tatu kutoka kushoto akiwa kwenye picha ya pamoja na wazee waliojitokeza kupatiwa huduma za upasuaji wa macho waliokuwa na matatizo ya mtoto wa Jicho
 MKUU wa wilaya ya Muheza Mkoani Tanga,Hajat Mhandisi Mwanasha Tumbo wa pili kulia akimkabidhi msaada wa vyakula mbalimbali mwakilishi wa wazee waliofanyiwa upasuaji wa macho ili viweze kuwasaidia baada ya kumalizika upasuaji huo watakapokwenda majumbani mwao wanaoshuhudia kulia ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Muheza,Luiza Mlelwa ,Mganga Mkuu wa Halmashauri hiyo,Mathew Mganga wa kwanza kushoto ni Katibu Tawala wa wilaya ya Muheza
Desderia Haule
Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Muheza,Luiza Mlelwa akipongezwa na mwakilishi wa wazee hao mara baada ya Mkuu wa wilaya hiyo,Mhandisi,Hajat Mwanasha Tumbo wa pili kulia kuwakabidhi vyakula vitakavyowasaidia watakapotoka kwenye matibabu hayo na kurejea makwao.
Na Blog ya Kijamii ya Tanga Raha

No comments:

Powered by Blogger.