MAKUBALIANO YA SOKO LA AFRIKA MASHARIKI BADO NI CHANGAMOTO.
Ikiwa Una Habari, Tukio, Picha, Maoni au Tangazo, Wasiliana Na BMG Kwa Nambari za Simu 0757 432694 Au Email binagimediagroup@gmail.com
James Salvatory, Dar
Imeelezwa kuwa bado kuna changamoto katika makubaliano yaliyowekwa mwaka 2010 katika nchi za ukanda wa Afrika Mashariki hususani kwenye Soko la pamoja la ukanda huo.
Hayo yamesemwa leo jijini Dar es salaam na Mkurugenzi wa Sera kutoka Taasisi ya sekta binafsi (TPSF) Gillad Teri kwenye mkutano uliowakutanisha wanachama wa sekta binafsi na kampuni zinazofanya kazi kwenye soko la Afrika Mashariki.
Amesema kuwa kulikuwa na makubaliano yaliyowekwa 2010 kwa kuruhusu uhuru wa mitaji ,bidhaa na watu kuvuka kwa nchi za afrika mashariki na katika hayo makubaliano yalikuwepo, makubaliano madogo 2700 ambayo nchi inapaswa kurekebisha ni pamoja na sheria,mifumo na utaratibu kwa lengo la kusaidia kukuza biashara na utengamano kwa nchi za afrika mashariki
Aidha amesema kuwa mkutano wa leo una lengo la kuchambua na kutadhimini kwa yale makubaliano yaliyowekwa miaka saba iliyopita kwa nchi za afrika mashariki kama yanatekelezeka ili kuweza kuwasilisha kwa serikali kwa zile changamoto zinazojitokeza hususani kwenye sheria.
James Salvatory, Dar
Imeelezwa kuwa bado kuna changamoto katika makubaliano yaliyowekwa mwaka 2010 katika nchi za ukanda wa Afrika Mashariki hususani kwenye Soko la pamoja la ukanda huo.
Hayo yamesemwa leo jijini Dar es salaam na Mkurugenzi wa Sera kutoka Taasisi ya sekta binafsi (TPSF) Gillad Teri kwenye mkutano uliowakutanisha wanachama wa sekta binafsi na kampuni zinazofanya kazi kwenye soko la Afrika Mashariki.
Amesema kuwa kulikuwa na makubaliano yaliyowekwa 2010 kwa kuruhusu uhuru wa mitaji ,bidhaa na watu kuvuka kwa nchi za afrika mashariki na katika hayo makubaliano yalikuwepo, makubaliano madogo 2700 ambayo nchi inapaswa kurekebisha ni pamoja na sheria,mifumo na utaratibu kwa lengo la kusaidia kukuza biashara na utengamano kwa nchi za afrika mashariki
Aidha amesema kuwa mkutano wa leo una lengo la kuchambua na kutadhimini kwa yale makubaliano yaliyowekwa miaka saba iliyopita kwa nchi za afrika mashariki kama yanatekelezeka ili kuweza kuwasilisha kwa serikali kwa zile changamoto zinazojitokeza hususani kwenye sheria.
No comments: