LIVE STREAM ADS

Header Ads

MASHABIKI WA SIMBA SC MWANZA WAWAANDALIA WACHEZAJI NA VIONGOZI WA TIMU HIYO CHAKULA CHA USIKU

Wasiliana na BMG kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma za Habari na Mangazo.

Binagi Media Group
Msemaji wa Simba Haji Manara amesema timu hiyo haina mpango wa kuachana na kocha wake mkuu Joseph Omogi na kukanusha uvumi mitandaoni kwamba kocha huyo ametakiwa kushinda mechi tano zijazo, lasivyo atatimliwa.

"Simba bado ni timu bora chini ya kocha Omogi, na niwaambieni tu kwamba Simba inamhitaji zaidi Omogi, kuliko Omogi anavyoihitaji Simba". Alisema Manara huku akisisitiza kwamba hitaji la Simba msimu huu ni kikombe na si vinginevyo.

Aliyasema hayo jana jijini Mwanza wakati akizungumza na wanahabari kuhusu maandalizi ya timu hiyo iliyoweka kambi Jijini humo ikiwa ni maandalizi ya kuelekea kwenye mchezo wa jumapili dhidi ya Stand United mkoani Shinyanga ambapo alisema kikosi kiko vizuri na hakina majeruhi.


Baadaye mashabiki wa Simba SC Jijini Mwanza (Rock City Simba SC Funs) waliwandalia wachezaji na viongozi wa timu hiyo chakula cha usiku ambapo Mwenyekiti wa mashabiki hao Bittony Mwakisu alisema mashabiki wana imani na timu yao hivyo ipambane kuhakikisha inanyakua ubingwa katika msimu huu.

Msemaji wa Simba SC, Haji Manara alizungumza mambo mengi ikiwemo mikakati ya timu ambayo itaifanya kuwa timu bora na tajiri huku akisisitiza pia msimamo wa timu hiyo juu ya kocha Omogi.
Hafla hiyo ilifanyika Diamond Hotel.
Mmoja wa mashabiki wa Simba SC Jijini Mwanza, Filbert Kabago.
Mwenyekiti wa Rock City Simba SC Funs, Bittony Mwakisu akizungumza kwenye hafla hiyo.
Mwenyekiti wa Rock City Simba SC Funs, Bittony Mwakisu akizungumza kwenye hafla hiyo.
Msemaji wa Simba, Haji Manara akizungumza kwenye hafla hiyo.
BMG Habari, Pamoja Daima!

No comments:

Powered by Blogger.