LIVE STREAM ADS

Header Ads

Salamu za mbunge wa Nyamagana kwa Rais Magufuli

Wasiliana na BMG kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma za Habari na Mangazo.

Na Binagi Media Group
Rais Dkt.John Pombe Magufuli jana alianza ziara ya kikazi ya siku mbili Jijini Mwanza ambapo alizindua daraja la juu la watembea kwa miguu la Furahisha, kuzindua kiwanda cha vinywaji baridi cha Sayona pamoja na kuwahutubia wananchi katika uwanja wa Mwatex.

Miongoni mwa viongozi waliopata fursa ya kuwasilisha salamu zao mbele ya Rais Magufuli ni pamoja na mbunge wa jimbo la Nyamagana, Stanslaus Mabula ambaye alifunguka mambo mengi ya kimaendeleo yaliyofanywa katika uongozi wake.

Baadaye Rais Magufuli alizungumza na wananchi na kusema kwamba amedhamiria kuibadilisha Tanzania kupitia mkakati wake wa ujenzi wa viwanda ambao utaimarisha uchumi pamoja na kutoa ajira nyingi kwa vijana huku akiwataka viongozi Jijini Mwanza kuungana pamoja kumaliza miogogoro waliyonayo hii ikiwa ni baada ya kupata taarifa ya kukamatwa kwa Meya wa Jiji la Mwanza, James Bwire, alipowasili kwenye uwanja wa ndege.

Bonyeza HAPA habari zaidi

No comments:

Powered by Blogger.