Makamu wa Rais ahitimisha ziara yake mkoani Songwe
Wasiliana na BMG kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma za Habari na Mangazo.
Imeandaliwa na Songwe RS
Makamu wa
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Samia Suluhu Hassan amehitimisha
ziara ya siku tano Mkoani Songwe mapema leo na kusisitiza ushirikiano baina ya
uongozi ili kuharakisha maendeleo.
Mhe.Samia
Suluhu Hassan amesema akiwa ziarani katika wilaya za Momba, Mbozi na Ileje
amebaini kuwa Mkoa wa Songwe umebarikiwa kuwa na rasilimali na utajiri mkubwa
kinachotakiwa ni viongozi kushirikiana katika kuwatumikia wananchi.
“Nimefurahishwa
na kaulimbiu yenu ya maendeleo yataletwa na sisi wenyewe kwa ushindani na
ushirikiano, bila ushirikiano hakuna maendeleo, kauli mbiu hii sasa ionekane
kwa vitendo”, amesisitiza.
Ameongeza
kwa kuwataka watendaji na viongozi wote wapende kuwatembelea wananchi kuanzia
ngazi za vijiji ili waweze kuwahudumia vizuri na sio kukaa ofisini.
Mhe Samia
Suluhu Hassan ameongeza kwa kuzitaka halmashauri kutenga fedha kwa ajili ya
kuwakopesha wanawake na vijana na kubuni miradi mikubwa itayaowaunganisha
wajasiriamali wanawake na vijana kutengeneza viwanda ili kuondokana na
umasikini.
Amesema
mpango wa mkoa wa kuanzisha vituo vya maendeleo vya kata utawezekana na
kuwanufaisha wananchi endapo watendapo watajitoa kwa dhati kuufanikisha na
mpango huu utaiwezesha Songwe kupaa kiuchumi.
Aidha Mhe
Samia Suluhu Hassan amewataka wananchi wa Mkoa wa Songwe kuendelea kutunza
mazingira kwa kupanda miti na wale walioko mipakani kuendelea kutunza amani.
Naye Mkuu wa
Mkoa wa Songwe Chiku Gallawa ameshukuru Mhe Samia Suluhu Hassan kwa kufanya
ziara mkoani Songwe kuahidi kuwa maelekezo na maagizo aliyoyatoa atayasimamia
yatekelezwe.
No comments: