LIVE STREAM ADS

Header Ads

Haruna Moshi kuivusha African Lyon Ligi Kuu

Wasiliana na BMG kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma za Habari na Mangazo.


Judith Ferdinand, BMG
Meneja wa timu ya African Lyon Adam Kipatacho amesema anaamini  mchezaji wao Haruna Moshi  ataisaidia timu hiyo kufanya vizuri katika msimu huu wa Ligi Kuu Tanzania Bara.

Akizungumza na majira jijini Mwanza Kipatacho alisema, Moshi ana nafasi  kubwa katika kuisaidia timu hiyo, kwani umri wake siyo mkubwa kama watu wanavyodhani wa kushindwa kusakata kabumbu.

Moshi katika mchezo wa raundi ya pili ya ligi kuu uliowakutanisha na Alliance FC ya jijini Mwanza aliifungia timu hiyo goli moja dakika ya nane, na kufanya hadi dakika tisini kumalizika kutoka sare ya goli 1-1.

Mchezaji huyo aliyewai kuichezea timu ya Moro United na Simba SC miaka kadhaa, ndiye pekee aliyeweza kuifungia timu yake goli tangu kuanza kwa ligi msimu huu.

Alisema, kuelekea mchezo wa raundi ya tatu dhidi ya Kagera Sugar  utakaochezwa septemba Mosi katika uwanja wa Kaitaba wamejipanga vizuri, anaamini wataibuka na point tatu hivyo kurejea Dar wakiwa na point nne kutoka Kanda ya Ziwa baada ya kupoteza mchezo wao wa kwanza waliocheza na Stand United ya mkoani Shinyanga.

"Mchezo haukuwa mbaya sana tumeyapokea matokeo hayo kwa sababu sisi tulikuja kutafuta point moja ndio lengo letu haswaa hivyo Kagera ndio tunaenda kumaliza gemu tutarejea dar tukiwa na point 4," alisema Kipatacho.

No comments:

Powered by Blogger.