LIVE STREAM ADS

Header Ads

Wizara ya afya yahimizwa kuongeza miuda ugawaji dawa za minyoo na kichocho

Wasiliana na BMG kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma za Habari na Mangazo.


Judith Ferdinand, BMG
Wizara ya Afya kupitia mpango wa kudhibiti magonjwa yaliyokuwa hayapewikKipaumbele (NTD), imehimizwa kuongeza muda wa zoezi la ugawaji dawa za minyoo na kichocho ili kufikia walengwa wengi.

Mratibu wa magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele kutoka Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela, Gisela Orasa amesema kuna changamoto mbalimbali zinazopelekea zoezi la ugawaji dawa za kichocho na minyoo shuleni kutofanikiwa kwa asilimia mia ikiwemo ufinyu wa siku.

Alisema zoezi la ugawaji dawa limekuwa likifanyika  kwa siku moja ambapo kwa mwaka huu limefanyika Agosti sita, hali inayopelekea kutofanikiwa kwa asilimia mia kwani walilenga kuwafikia wanafunzi 94,743 kutoka shule za msingi 116 na waliomeza dawa  ni 84,417.

"Kuna baadhi ya wanafunzi hawakufika shuleni siku ya zoezi la ugawaji dawa za magonjwa ya kichocho na minyoo kutokana na sababu mbalimbali ni bora wizara husika ikaongeza  siku  angalau zikawa tatu ambapo mtoto ambaye hakumeza siku ya kwanza atapewa siku ya pili au ya tatu”. Alisema Orasa.

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela Dkt. Florian  Tinuga alisema mkakati walionao katika kudhibiti magonjwa hayo ni kuingiza kwenye bajeti ya wilaya ambapo kwa sasa wanayapa kipaumbele kwani wanahitaji fedha za kutosha ili kuwafikia wananchi.

Alisema mwaka ujao wataanza zoezi la uhamasishaji mapema  pamoja na kuweka  mfumo mmoja ambao utakuwa kwa shule zote zilizopo katika halmashauri hiyo kwa kukaa na wazazi na kupendekeza ni namna gani watachangia chakula ili kufanikisha zoezi hilo kwa asilimia mia na watoto wanameza dawa hizo.

No comments:

Powered by Blogger.