Mwenge ulivyokagua hatua kwa hatua miradi ya maendeleo Misungwi
Wasiliana na BMG kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma za Habari na Mangazo.
Ujumbe wa kusisimua kutoka kwa wanafunzi wenye ulemavu
Mwenge wa
Uhuru wilayani Misungwi umekagua, kuweka mawe ya msingi na kuzindua miradi
minane ikiwemo ya afya, barabara, ufugaji samaki na maji yenye thamani ya
shilingi bilioni 2.3
Kiongozi wa mbio za Mwenge Kitaifa Charles Kabeho na ujumbe wake wakikagua matengenezo ya barabara ya Misungwi-Bomani kabla ya kufanya uzinduzi wa barabara hiyo iliyojengwa kwa kiwango cha moramu
Kiongozi wa mbio za Mwenge Kitaifa Charles Kabeho akikata utepe kuashiria uzinduzi wa mradi wa mabawa ya samaki Sawenge
Ujumbe wa mbio za mwenge pia umechoma nyavu haramu baada ya kuzindua mabwawa ya samaki Sawenge
Kiongozi wa mbio za Mwenge Kitaifa Charles Kabeho akizungumza na wanafunzi wanaounda Klabu ya wapinga rushwa katika shule ya upili ELPASS baada ya kuweka jiwe la msingi kwenye shule hiyo
Kiongozi wa mbio za Mwenge Kitaifa Charles Kabeho pia alikabidhi mikopo inayotolewa na Halmashauri kwa vikundi vya akina mama, vijana na walemavu yenye thamani ya shilingi milioni 50
Mwenge wa Uhuru uliweka jiwe la msingi kwenye mradi wa ujenzi wa jengo la baba, mama na mtoto OPD katika Hospitali ya Wilaya Misungwi
Kiongozi wa mbio za Mwenge Kitaifa Charles Kabeho pia likabidhi zawadi za kombe kwa washindi wa ligi ya Mwenge Cup 2018 wilayani Misungwi
Shirika la KIVULINI ni miongoni mwa wadau walioshiriki mapokezi ya mbio za Mwenge wilayani Misungwi
Mkuu wa Wilaya Misungwi Mhe. Juma Sweda (kulia) akikabidhi taarifa ya Mwenge ya wilaya hioyo kwa kiongozi wa mbio za Mwenge kitaifa Charles Kabeho
Ujumbe wa kusisimua kutoka kwa wanafunzi wenye ulemavu
No comments: