LIVE STREAM ADS

Header Ads

Ibungilo watinga robo fainali michuano ya Angeline Jimbo Cup wilayani Ilemela

Wasiliana na BMG kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma za Habari na Mangazo.


Judith Ferdinand, BMG
Timu ya Ibungilo imeendeleza kutoa kipigo baada ya kuifunga Nyamanoro goli 4-0 katika mashindano ya Angeline Jimbo Cup msimu wa 2018/19 yanayoendelea kutimua vumbi katika  viwanja mbalimbali wilayani Ilemela.

Katika mchezo uliochezwa jana kwenye uwanja wa Kona ya Bwiru na kukutanisha timu kutoka kundi A, ambapo Nyamanoro ilionekana kuzidiwa mashambulizi na hadi dakika tisini walishindwa kutikisa nyavu za Ibungilo.

Timu ya Ibungilo ilifunga magoli kupitia washambuliaji wake Said Said magoli matatu na Didas Msafiri goli moja, hivyo kufanya timu hiyo kuongoza katika kundi hilo kwa kuwa na jumla ya pointi kumi huku wakishinda mechi tatu na sare moja.

Akizungumza baada ya kumalizika kwa mchezo huo, Kocha wa Ibungilo Swala Daud alisema alishukuru kwa matokeo aliyopata kwani mpaka sasa timu yake imefuzu kutinga hatua ya nane bora (robo fainali).

Alisema timu yake inafanya vizuri japo yapo mapungufu madogo ambayo atayafanyia kazi ili kuweza kufuzu kuingia fainali na kuibuka mabingwa wa msimu huu kwani ndio lengo huku aliwashukuru mashabiki wa timu hiyo na kuwaomba waendelee kuiunga mkono kwani hatua inayofuatia ni ngumu zaidi na watakutana na mabingwa wa hatua ya makundi.

Katika mchezo mwingine uliochezwa katika uwanja wa Buswelu, timu ya Kata ya Mecco imeibuka na ushindi wa goli 3-1 dhidi ya Kahama kupitia kwa washambuliaji wake Paul Charles, Sylvester Godfrey na Lucas Anderson huku Kahama wakipata goli la kufutia machozi kupitia kwa Legan Legan.

No comments:

Powered by Blogger.