LIVE STREAM ADS

Header Ads

Kampuni ya Mwanza Huduma yaungana mkono juhudi za mbunge wa Nyamagana

Wasiliana na BMG kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma za Habari na Mangazo.

Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
Kampuni ya Mwanza Huduma imeunga mkono juhudi za maendeleo za mbunge wa jimbo la Nyamagana Mhe.Stanslaus Mabula (CCM), kwa kumkabidhi mifuko 230 ya saruji ili kusaidia ujenzi wa miradi mbalimbali ikiwemo ya elimu.

Akikabidhi mifuko hiyo leo, Mkurugenzi wa kampuni hiyo Zulfikar Nanji ametoa rai kwa wafanyabiashara wengine kusaidia shughuli mbalimbali za maendeleo badala ya kuitegemea serikali pekee.

Akipokea mifuko hiyo, Mhe.Mabula ameishukuru kampuni hiyo kwa kuendelea kusaidia miradi ya maendeleo katika jimbo la Nyamagana na kwamba mifuko hiyo itasaidia kukamilisha shughuli za ujenzi katika sekta ya elimu na afya jimboni Nyamagana.

Naye Mwenyekiti wa taasisi ya maendeleo ya First Community, Ahmed Misanga ametoa pongezi kwa mbunge Mabula pamoja na kampuni ya Mwanza Huduma kupitia kwa Mkurugenzi wake Zulfikar Nanji kwa ushirikiano huo ambao unaunga mkono juhudi za serikali ya awamu ya tano za kufikisha maendeleo kwa wananchi.
Mkurugenzi wa kampuni hiyo Zulfikar Nanji (kushoto) akimkabidhi mifuko 230 ya saruji (simenti) mbunge wa jimbo la Nyamagana Mhe.Stanslaus Mabula (wa tatu kulia) kwa ajili ya kuunga mkono juhudi za maendeleo jimbo la Nyamagana

No comments:

Powered by Blogger.