Kampuni ya Mwanza Huduma yaungana mkono juhudi za mbunge wa Nyamagana
Wasiliana na BMG kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma za Habari na Mangazo.
Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
Kampuni ya
Mwanza Huduma imeunga mkono juhudi za maendeleo za mbunge wa jimbo la Nyamagana
Mhe.Stanslaus Mabula (CCM), kwa kumkabidhi mifuko 230 ya saruji ili kusaidia
ujenzi wa miradi mbalimbali ikiwemo ya elimu.
Akikabidhi
mifuko hiyo leo, Mkurugenzi wa kampuni hiyo Zulfikar Nanji ametoa rai kwa
wafanyabiashara wengine kusaidia shughuli mbalimbali za maendeleo badala ya kuitegemea
serikali pekee.
Akipokea
mifuko hiyo, Mhe.Mabula ameishukuru kampuni hiyo kwa kuendelea kusaidia miradi
ya maendeleo katika jimbo la Nyamagana na kwamba mifuko hiyo itasaidia
kukamilisha shughuli za ujenzi katika sekta ya elimu na afya jimboni Nyamagana.
Naye
Mwenyekiti wa taasisi ya maendeleo ya First Community, Ahmed Misanga ametoa
pongezi kwa mbunge Mabula pamoja na kampuni ya Mwanza Huduma kupitia kwa
Mkurugenzi wake Zulfikar Nanji kwa ushirikiano huo ambao unaunga mkono juhudi
za serikali ya awamu ya tano za kufikisha maendeleo kwa wananchi.
Mkurugenzi wa kampuni hiyo Zulfikar Nanji (kushoto) akimkabidhi mifuko 230 ya saruji (simenti) mbunge wa jimbo la Nyamagana Mhe.Stanslaus Mabula (wa tatu kulia) kwa ajili ya kuunga mkono juhudi za maendeleo jimbo la Nyamagana
No comments: