LIVE STREAM ADS

Header Ads

Matokeo: Michuano ya Angeline Cup 2018

Wasiliana na BMG kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma za Habari na Mangazo.

Judith Ferdinand, Mwanza
Timu ya soka ya Kata ya Kirumba imeilaza timu ya Kata ya Nyamanoro kwa  goli 1-0 katika mwendelezo wa mashindano ya Angeline Jimbo Cup 2018 yanayoendelea  kutimua vumbi katika viwanja mbalimbali wilayani Ilemela.

Mchezo huo uliotumua vumbi katika  uwanja wa Kona ya Bwiru ulikutanisha timu kutoka kundi A ambapo Kirumba ilifunga goli kupitia mshambuliaji wake Boniphace Katengasi dakika 51.

Akizungumzia mchezo huo , diwani wa Kata ya Kirumba Alex Ngusa aliipongeza timu yake kwa kuibuka na ushindi huo huku akisema watafanya vizuri katika mechi zijazo kwani ndio wameanza kuwasha moto licha ya kwamba waliweza kupoteza kwenye mechi ya kwanza ya uzinduzi baada ya kukubali kichapo cha goli 1-0 dhidi ya Kata ya Ibungilo.

Ngusa alisema wachezaji wanatakiwa kuzingatia nidhamu kwani ndio msingi wa kufanikiwa katika soka huku akimpongeza mbunge wa jimbo lA Ilemela Angeline Mabula na kamati yake ya maandalizi kwa kuandaa mashindano hayo maalum kwa ajili ya kuibua vipaji vya soka kwa vijana wa jimbo hilo kama Ilani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) inavyoelekeza.

Kwa upande wake Nahodha wa timu ya Nyamanoro, Khuzaifa Ibrahim alisema wamepoteza mchezo huo na wataenda kufanyia kazi mapungufu na makosa yaliyojitokeza ili Michezo ijayo wafanye vizuri huku akiwaomba wapenzi wa timu hiyo waendelee kuinga mkono na kujitokeza viwanjani kushangilia.

Hata hivyo katika mchezo mwingine  timu ya Kata ya Ilemela  ilitoa kichapo cha goli  2-1 dhidi ya Kata ya Kiseke, mchezo uliochezwa  uwanja wa Sabasaba na kukutanisha timu kutoka kundi C.

Timu ya Ilemela ilifunga magoli kupitia Joseph John dakika ya sita na Emanuel Samuel dakika ya 32 huku Kiseke ikipata goli kupitia mshambuliaji wake Edwin Robert dakika ya 12 huku katika mchezo wa tatu uliochezwa uwanja we Buswelu Kati ya timu ya Kata ya Buswelu na Kata ya Mecco zikitoka suluhuu  ya bila kufungana.

No comments:

Powered by Blogger.