Mkurugenzi Alliance amwomba RC Mongella kuzinusuru timu za Mwanza
Wasiliana na BMG kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma za Habari na Mangazo.
Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
Mkuu wa Mkoa
wa Mwanza Mhe.John Mongella amezungumza na wachezaji wa timu ya Alliance FC
ikiwa zimesalia siku chache kuelekea Agosti 22, 2018 ambapo msimu wa ligi kuu
Tanzania Bara utaanza rasmi.
Mhe.Mongella
amewapa ari kubwa wachezaji wa timu hiyo inayoshiriki ligi kuu kwa mara ya
kwanza katika msimu huu wa mwaka 2018/19 na kuwataka wahakikishe wanaifunga
kila timu wanayokutana nayo.
Hata hivyo
Mkurugenzi wa Alliance FC, James Bwire amemuomba Mhe.Mongella kuzisaidia timu
za Jijini Mwanza zinazoshiriki ligi kuu kwa kuitisha kikao cha wadau wa soka
pamoja na wawekezaji mbalimbali wenye fursa ya kudhamini timu hizo.
Katika
mchezo wa kwanza, Alliance FC itamenyana vikali na mahasimu wao wa soka Mbao FC
katika uwanja wa CCM Kirumba, Agosti 22, 2018 ambapo hadi sasa joto la mchezo
huo limezidi kupanda miongoni mwa timu zote mbili pamoja na mashabiki Jijini
Mwanza.
Mkurugenzi
wa timu ya Alliamce FC, James Bwire akizungumza baada ya Mkuu wa Mkoa Mwanza
Mhe.John Mongella kuitembelea timu hiyo
Mwenyekiti
Kamati ya Mashindano timu ya Alliance DC, Yusuph Budodi akiwasilisha salamu
zake
Baadhi wa
wachezaji wa Alliance FC
Tazama BMG Online Tv hapa chini
No comments: