MWANZA- Huduma ya maji kupatikana kama umeme wa luku
Wasiliana na BMG kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma za Habari na Mangazo.
Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
Waziri wa
Maji na Umwagiliaji Mhe.Profesa Makame Mbarawa amezindua mpango wa kufunga mita
za maji za “malipo kabla” ambapo watumiaji wa maji watakuwa wakifanya malipo
kwa njia ya benki ama mitandao ya simu za rununu kabla ya kuanza hutumia huduma
hiyo.
Mhe. Profesa
Mbarawa alifanya uzinduzi huo jana na kubainisha kwamba mpango huo utasaidia
kuondoa malalamiko ya watumiaji wa maji kubambikiziwa bili huku pia ukisaidia
serikali kukusanya mapato stahiki.
Hata hivyo Mkurugenzi
wa Mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira mkoani Mwanza (MWAUWASA), Mhandisi
Antony Sanga alisema kwa sasa huduma hiyo inatolewa kwa viongozi wa serikali na
taasisi mbalimbali ikiwemo viwanda kabla ya kuwafikia wananchi wote.
Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mhe.Profesa Makame Mbarawa akisalimiana na wafanyakazi wa MWAUWASA
No comments: