Michuano ya Angeline Cup 2018 yazidi kupamba moto wilayani Ilemela
Judith Ferdinand, BMG
Michuano ya
Angeline Cup 2018 imeendelea kutimua vumbi katika viwanja mbalimbali wilayani
Ilemela ambapo jana timu ya Kata ya Ibungilo iliichabanga timu ya Kata ya
Pasiansi bao 3-1.
Katika
mchezo huo uliochezwa katika uwanja wa Kona ya Bwiru ukihusisha timu kutoka
kundi A, Ibungilo walipata magoli yao kupitia kwa washambuliaji wake Michael
George aliyefunga goli moja na Said Said aliyepachika magoli mawili.
Mchezo mwingine
uliochezwa wenye uwanja wa Buswelu na ukikutanisha timu za kundi B ambapo Nyakato ilitoa kichapo cha goli 1-0
dhidi ya Kahama kupitia mshambuliaji wake Hamada Mtegeta.
Timu ya
Shibula imeilaza Kayenze kwa magoli 3-2 katika mchezo uliochezwa kwenye uwanja
wa shule ya msingi Bugongwa na kukutanisha timu kutoka kundi D.
Wakati huo
huo Nyasaka imeiondoka na pointI tatu baada ya kuichapa Kawekamo goli 2-1 katika
mchezo uliochezwa kwenye uwanja wa Sabasaba ukikutanisha timu kutoka kundi C.
Ikumbukwe
kuwa mashindano hayo yalizinduliwa Agosti 11, 2018 ambapo yameandaliwa na Mbunge wa Jimbo la Ilemela, Angeline
Mabula yakishirikisha timu 19 kutoka Kata zote za wilayani Ilemela kwa lengo la
kuibua vipaji kwa vijana.
No comments: