LIVE STREAM ADS

Header Ads

RC Mwanza ameguswa inshu ya wanafunzi kusomea nje

Wasiliana na BMG kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma za Habari na Mangazo.

Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
Mkuu wa Mkoa Mwanza Mhe.John Mongella ameguswa na suala la upungufu wa vyumba vya madarasa katika shule ya msingi Nkumba iliyopo wilayani Sengerema na kuungana na wananchi kuchangia ujenzi wa vyumba vitatu vya madarsa shuleni hapo.

RC Mongella amefanya ziara katika shule hiyo akiambatana na viongozi mbalimbali akiwemo Mkuu wa Wilaya Sengerema, Mkurugenzi Halmashauri ya Sengerema, Kamati ya Ulinzi na Usalama Mkoa Mwanza na kuendesha harambee ya papo kwa hapo ili kiufanikisha ujenzi huo.

Katika harambee hiyo, shilingi 710,000 zilipatikana pamoja na ahadi ya mifuko minane ya saruji, tripu mbili za mchanga, debe nne za mpunga, kuku watatu pamoja na debe moja la mchembe lengo likiwa ni kuwanusuru zaidi ya wanafunzi 200 wanaosomea nje.

Pia RC Mongella amekagua miradi mbalimbali ya maendeleo wilayani Sengerema ikiwemo mradi wa kisima Kisoli, ghala la chakula Isole, ujenzi wa maabara, jengo la upasuaji, chumba cha kuhifadhia maiti, nyumba ya mtumishi, wodi ya baba, mama na mtoto katika Kituo cha Afya Kagunga.
Vyumba vya madarasa vinavyojengwa katika shule ya msingi Nkumba wilayani Sengerema
Ghala la chakula katika Kijiji cha Isole

No comments:

Powered by Blogger.