BUKOMBE: Waziri Mwakyembe ahitimisha Mashindano ya Doto Cup 2018
Wasiliana na BMG kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma za Habari na Mangazo.
SOMA>>>Biteko achangia ujenzi wa shule mbili Bukombe, ajibu kero ya umeme
Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
Waziri wa
Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe amekabidhi zawadi
kwa washindi wa mashindano ya “Doto CUP 2018” yaliyofikia tamati jana katika
uwanja wa shule ya msingi Uyovu, wilaya ya Bukombe mkoani Geita.
Kwa upande
wa soka (wakubwa), timu ya Ushirombo Renjaz (Rangers) iliibuka mshindi baada ya
kuichabanga timu ya Lyamba Mgongo bao 2-0 na kujinyakulia kitita cha shilingi
laki tano, jezi seti tatu, mipira mitatu pamoja na kombe.
Mshindi wa
pili timu ya Lyamba Mgongo ilijinyakulia shilingi laki tatu, jezi seti mbili na
mipira mitatu huku mshindi wa tatu timu ya Kazibizyo FC akijinyakulia shilingi
laki mbili, jezi seti moja na mpira mmoja.
Kwa upande
wa watoto, timu za Simba na Yanga zilitoshana nguvu kwa sare ya bao 1-1 na
hivyo kila timu kujinyakulia shilingi 25,000 huku mfungaji bora Carol Frances na
mlinda mlango bora Casto Paul wote wakiibuka na shilingi elfu hamsini kila
mmoja.
Michezo
mingine ilikuwa ni kuvuta kamba ambapo kwa upande wa wanaume Simba waliibuka
mshindi dhidi ya Yanga na kujinyakulia shilingi elfu hamsini huku upande wa
wanawake Yanga wakiibuka washindi dhidi ya Simba na kujishindia shilingi elfu
hamsini pia.
Kwenye
mchezo wa Karate, Shotokan walijishindia elfu hamsini, mpira wa wavu PVC
walijishindia elfu hamsini, mbio za mita 100 wanaume mshindi alikuwa Projestus
Rutha na wanawake ushindi ulienda kwa Tumain Mwasilembo ambapo kila mmoja alijinyakulia
shilingi elfu hamsini, mpira wa pete timu ya Kurugenzi alijinyakulia pia
shilingi elfu hamsini.
Mbio za
baiskeli mshindi mshindi wa kwanza Furaha Joseph alijinyakulia elfu sitini na
mshindi wa pili Subi Kachila akijishindia shilingi elfu 40, mbio za magunia upande
wa wanaume mshindi alikuwa Daniel Ishike na wanawake alikuwa Linda Deo ambapo
kila mmoja alijishindia shilingi elfu hamsini huku mbio za kuku wanaume na
wanawake kila mshindi akiondoka na kuku.
Akizungumza
kwenye fainali za mashindano hayo, Waziri Dkt. Mwakyembe alikiri suala la ubovu
wa viwanja vya michezo katika halmashauri mbalimbali nchini ikiwemo Bukombe na kutoa
rai kwa halmashauri kuweka mikakati ya kuboresha viwanja hivyo na kwamba serikali
itaunga mkono juhudi hizo ili kuhakikisha vinakuwa bora kwani michezo ni ajira.
Mashindano
hayo yalianza Julai 27, 2018 yakiandalia na mbunge wa jimbo la Bukombe, Doto
Mashaka Biteko (CCM) ambaye pia ni Naibu Waziri wa Madini yakiwa na lengo la
kuibua na kuendeleza vipaji, kuchochea maendeleo na kuimarisha umoja huku
kaulimbiu ikiwa ni “Kusema na Kutenda”.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe akizungumza kwenye fainali za mashindano ya Doto Cup 2018 ambapo alikuwa mgeni rasmi.
Mwandaaji wa mashindano ya Doto Cup, Doto Mashaka Biteko ambaye ni mbunge wa jimbo la Bukombe na pia Naibu Waziri wa Madini akizungumza kwenye fainali za mashindano hayo.
Mkuu wa Wilaya Bukombe mkoani Geita, Mhe. Said Nkumba akitoa salamu zake kwenye fainali za mashindano hayo
Mbunge wa jimbo la Geita Mjini, Costantine Kanyasu akitoa salamu zake
Mbunge wa jimbo la Kahama, Jumanne Kishimba akiwasilisha salamu zake
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe, akikabidhi zawadi ya kombe kwa timu ya Ushirombo Rangers baada ya kuibuka mshindi wa kwanza
Washindi wakifurahia ushindi wao
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe, akikagua timu za mpira wa pete
Mwandaaji wa mashindano ya Doto Cup, Doto Mashaka Biteko ambaye ni mbunge wa jimbo la Bukombe na pia Naibu Waziri wa Madini akisalimiana na wachezaji
Tazama BMG Online Tv hapa chini
SOMA>>>Biteko achangia ujenzi wa shule mbili Bukombe, ajibu kero ya umeme
No comments: