LIVE STREAM ADS

Header Ads

Mwanza wapania kuendeleza mchezo wa kikapu

Wasiliana na BMG kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma za Habari na Matangazo.

Judith Ferdinand, BMG
Wadau mbalimbali mkoani Mwanza  wametakiwa kuendeleza mchezo wa mpira wa kikapu (Basketball ), ili kuibua na kuendeleza vipaji vipya kutoka kwa vijana na kuuwakilisha mkoa katika mashindano mbalimbali ya kitaifa na kimataifa.

Mratibu wa Mpira wa Kikapu kwa watoto na vijana mkoani Mwanza, Bahati Kizito alitoa rai hiyo kwenye bonanza la mchezo huo lililoshirikisha shule za msingi na sekondari kutoka Nyamagana, Ilemela na Magu.

Kizito alisema, licha ya mafanikio walioyapata katika mchezo huo bado wanakabiliwa na upungufu wa vifaa pamoja na viwanja hivyo anaomba wadau kuwaunga mkono na kuendeleza mpira wa kikapu kwa kusaidia kutatua changamoto hizo.

Alisema, bonanza hilo ni sehemu ya programu ya uibuaji na uendelezaji wa mchezo huo, ambayo ipo katika baadhi ya mikoa nchini ikiwa chini ya mpango uitwao “Tanzania Youth Basketball Program”.

Pia alisema baada ya bonaza hilo, nguvu itaelekewa kwa wachezaji walioshiriki kuendelea na mazoezi kila siku baada ya muda wa masomo katika viwanja vilivyo karibu na maeneo wanayoishi ikiwemo Kiloleli, Mirongo, B.O.T, Pasiansi, Butimba TTC na Kirumba ambapo kutakuwa na makocha watakaokuwa wakiwafundisha ili kuwaimarisha zaidi.

Naye mbunge wa Nyamagana , Stanslaus Mabula  ambaye alikuwa mgeni rasmi kwenye bonanza hilo alisema michezo ni afya na ajira hivyo washiriki watumie nafasi hiyo  vizuri, huku jitihada za kuboresha miundombinu ya viwanja katika maeneo ya Sabasaba na Pamba zikiendelea.

Kwa upande Katibu na mwakilishi wa mbunge wa Ilemela Kanda ya Bugogwa, Rebeca Yusuph alisema mbunge wa jimbo hilo yuko tayari kushirikiana na wadau wa mchezo huo ili kuhakikisha wanaibua na kuendeleza vipaji vya vijana.

Katika bonanza hilo,  timu ya wasichana kutoka shule ya J-Mond iliibuka na ushindi dhidi ya Kiloleli huku wavulana Kiloleli ikiichapa Thaqaafa goli 10-8.

No comments:

Powered by Blogger.