Kiongozi wa Mwenge ataka mradi wa mzani Ilemela ukamilike haraka
Wasiliana na BMG kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma za Habari na Mangazo.
PIA SOMA Kiongozi wa mbio za Mwenge kitaifa atoa ujumbe mzito Ilemela
Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
Kiongozi wa
mbio za Mwenge kitaifa Ndg. Charles Kabeho amemwagiza mkandarasi kampuni ya M/S
Great Lakers ya Mwanza kuhakikisha anakamilisha kwa wakati mradi wa ujenzi wa mizani
Mwaloni Kirumba.
Kabeho
alitoa kauli hiyo jana kabla ya kuweka jiwe la msingi kwenye mradi huo
unaojengwa na Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela kwa gharama za shilingi
milioni 293, 268, 739 ikiwa ni fedha za ndani.
Alisema
kukamilika kwa mradi huo kutasaidia kupunguza malalamiko kutoka kwa
wafanyabiashara pamoja na kuongeza mapato ya serikali kuu na Manispaa ya Ilemela.
Taarifa ya
mradi huo inaonyesha utekelezaji ulianza Novemba 11, 2017 na ulitarajiwa
kukamilika Februari 22, 2018 lakini haukukamilika kwa wakati kutokana na sababu
mbalimbali ikiwemo kubadilishwa eneo la mradi na hivyo kusababisha kuongezeka
kwa kazi kutokana na aina ya udongo.
Miradi
mingine iliyopitiwa na Mwenge wa Uhuru ni pamoja na ufunguzi wa karakana ya
mafunzo ya ufundi wa umeme wa viwandani katika chuo cha VETA Mwanza uliogharimu
shilingi milioni 320,398,091.27, ufunguzi wa bweni la wasichana katika shule ya
sekondari Buswelu uliogarimu milioni 150,888,910, uwekaji jiwe la msingi kwenye
ujenzi wa Zahanati ya Lukobe uliogharimu milioni 46,615,000.
Pia uwekaji
jiwe la msingi kwenye ujenzi wa shule ya msingi Tarajali (Bugogwa B) ambao hadi
sasa umegharimu shilingi milioni 85, 872,000, ujenzi wa ofisi ya Kata Pasiansi
uliogharimu shilingi milioni 50,189,000 na ujenzi wa barabara ya
Kabuhoro-Ziwani yenye urefu wa kilomita 1.5 inayojengwa kwa kiwango cha lami na
kampuni ya Gemen Engineering kwa shilingi milioni 916,812,210.
PIA SOMA Kiongozi wa mbio za Mwenge kitaifa atoa ujumbe mzito Ilemela
No comments: