Mongella aeleza ni kwa nini Rais Magufuli anastahili mapokezi makubwa
Wasiliana na BMG kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma za Habari na Mangazo.
PIA SOMA Ratiba na shughuli atakazofanya Rais Magufu mkoani Mwanza
Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli
anatarajiwa kufanya ziara ya kikazi mkoani Mwanza jumatatu Septemba 03- 04,
2018.
Mkuu wa Mkoa
Mwanza Mhe. John Mongella amesema kesho Septemba 03, 2018 Mhe. Rais Dkt. Magufuli
atashuhudia utiaji saini mikataba ya ujenzi wa meli mpya, chelezo na ukarabati
wa meli za MV. Victoria na MV. Butiama ambapo hafla hiyo itafanyika katika eneo
la Bandari ya Mwanza Kusini kuanzia majira ya saa moja asubuhi.
Amesema
jumanne Septemba 04, 2018 majira ya saa mbili asubuhi, Mhe. Rais Dkt. Magufuli atazindua
kiwanda cha Lakairo Group of Companies kilichopo Kijiji cha Isangijo wilayani
Magu, majira ya saa sita atazindua mradi wa upanuzi wa Chuo cha Ualimu
Murutunguru wilayani Ukerewe.
Siku hiyo
hiyo majira ya saa nane mchana Mhe. Rais Dkt. Magufuli atazindua mradi wa maji
katika Kijiji cha Nebuye wilayani ukerewe na majira ya saa tisa mchana atazungumza
na wananchi kupita mkutano wa hadhara utakaofanyika katika uwanja wa Getrude
Mongella uliopo Nansio.
Mhe.
Mongella amewahimiza wananchi wote kujitokeza kwa wingi kumlaki Mhe. Rais Dkt.
Magufuli katika maeneo yote atakayopita kutokana na nia yake ya dhati katika
kuiletea Tanzania maendeleo.
PIA SOMA Ratiba na shughuli atakazofanya Rais Magufu mkoani Mwanza
No comments: