Wanahabari waliopata ajali wapokea salamu za Rais Magufuli kwa hisia kali
Wasiliana na BMG kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma za Habari na Matangazo.
SOMA Ziara ya Rais Magufuli mkoani Mwanza
Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli ametuma salamu za
pole kwa waandishi wa habari pamoja na watu wengine waliopata ajali katika
msafara wake uliokuwa ukielekea Ukerewe Septemba 04, 2018.
Salamu hizo
zimewasilishwa leo Septemba 07, 2018 na Mkuu wa Mkoa Mwanza Mhe. John Mongella
na kuongeza kwamba Mhe. Rais Magufuli anatambua mchango wa wanahabari hivyo
ameguswa na ajali hiyo.
Wakizungumza kwa hisia kali, baadhi ya wanahabari wamemshukuru Mhe. Rais kwa salamu zake.
SOMA Ziara ya Rais Magufuli mkoani Mwanza
No comments: