Kumbukizi ya Miaka 19 ya Baba wa Taifa Mwl. Nyerere
Wasiliana na BMG kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma za Habari na Mangazo.
Oktoba 14,
2018 ni kumbukizi ya miaka 19 tangu afariki dunia Mwasisi wa Taifa la Tanzania
na mpigania Uhuru wa Tanganyika pamoja na mataifa mbalimbali barani Afrika,
Hayati Mwl. Julius Kambarage Nyerere.
Katika kumbukizi
hii, Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli pamoja mkewe Mama Janeth Magufuli wamemtembelea
mjane wa Mwl. Nyerere, Mama Maria Nyerere anayeishi Msasani Jijini Dar es
salaam.
Mhe. Rais
Magufuli amesema serikali itaendelea kumuenzi Baba wa Taifa Hayati Mwl. Julius
Kambarage Nyerere kwa fikra na mipango mizuri aliyoiweka inatekelezwa kwa
manufaa ya watanzania wote.
Hayati Mwl.
Nyerere aliyezaliwa mwaka 1922, alifariki dunia Oktoba 14, 1999 akiwa nchini
Uingereza alikokuwa akipatiwa matibabu.
Mhe. Rais
Dkt. John Pombe Magufuli na mkewe Mama Janeth Magufuli walimtembelea mjane
wa Mwl. Nyerere, Mama Maria Nyerere nyumbani Msasani Jijini Dar es salaam.
Mhe. Rais
Magufuli akisalimiana na Mama Maria Nyerere.
Mama Janeth Magufuli akisalimiana na Mama Maria Nyerere.
Tazama BMG Online Tv hapa chini.
Picha na Ikulu & Habari Maelezo
No comments: