Mbunge Dkt. Ashatu Kijaji aeleza utekelezaji wa Ilani ya CCM jimbo la Kondoa
Wasiliana na BMG kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma za Habari na Mangazo.
Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
Mbunge wa
jimbo la Kondoa mkoani Dodoma, Dkt. Ashatu Kijaji amewahimiza wakazi wa jimbo
hilo kuendelea kushirikiana na serikali pamoja na wadau mbalimbali katika
kutekeleza shughuli na miradi ya maendeleo ikiwemo elimu, afya, maji pamoja na
miundombinu.
Dkt. Kijaju
alitoa rai hiyo jana wakati akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa Ilani ya
Uchaguzi wa Chama cha Mapinduzi CCM ya mwaka 2015/20 katika kipindi cha miaka
mitangu tangu achaguliwe kuwa mbunge wa jimbo hilo, kwenye Mkutano Mkuu Maalum
wa chama hicho wilaya ya Kondoa.
Katika sekta
ya maji, Dkt. Kijaju alisema visima 56 vimechimbwa na kukarabatiwa kwa fedha za
serikali na wadau wa maendeleo ambazo ni shilingi 1,808,075,696 hatua ambayo imesaidia
wakazi wa jimbo la Kondoa kuondokana na kero ya uahaba wa maji.
Alisema
ujenzi wa vyumba vya madarasa, nyumba za waalimu, vyoo bora, utengenezaji wa
madawati, ujenzi wa shule mpya, ukarabati wa shule za zamani pamoja na makambi
ya wanafunzi umesaidia kuongeza ufaulu katika sekta ya elimu kutoka asilimia 37
mwaka 2014 katika mtihani wa darasa la saba hadi asilimia 68 mwaka 2017.
Kwa upande
wa sekta ya afya, Dkt. Kijaji alisema vituo vipya vinne vya afya vimejengwa
huku kituo kimoja cha afya kikifanyiwa ukarabati mkubwa ambapo shilingi bilioni
2.3 zimetengwa kwa ajili ya kukamilisha uboreshaji wa sekta hiyo.
Alipongeza
juhudi serikali, wananchi na wadau wa maendeleo zilizofanyika katika kipindi
cha miaka mitatu na kufanikisha uboreshaji wa miundombinu ya barabara pamoja na
madaraja huku Vijiji vinane vikinufaika na umeme kupitia mpango wa REA II na
kwamba Vijiji 73 vinatarajia kunufaika na mpango huo katika awamu inayofuata.
Mkutano huo
ulihudhuriwa na viongozi mbalimbali pamoja na wajumbe zaidi ya elfu moja
wilayani Kondoa ambapo walifurahishwa na taarifa Dkt. Kijaji ambaye pia ni
Naibu Waziri wa Fedha na Mipango wakisema ni mfano bora unaopaswa kuigwa na
viongozi wengine.
Mbunge wa Kondoa, Dkt. Ashatu Kijaji (wa pili kushoto) pamoja na viongozi mbalimbali mkoani Dodoma wakiwa kwenye mkutano huo.
Sehemu ya wajumbe wa Mkutano Mkuu Maalum wa Chama cha Mapinduzi CCM wilayani Kondoa
Mbunge wa jimbo la Bukombe, Mwl. Doto Biteko ambaye pia ni Naibu Waziri wa Madini ni miongoni mwa viongozi waalikwa waliohudhuria mkutano huo, na hapa anawasilisha salamu zake.
Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Ajira, Vijana na Watu wenye Ulemavu Mhe. Antony Mavunde akiwasilisha salamu zake kwenye mkutano huo.
Naibu Waziri OR-TAMISEMI, Mhe. Joseph Kakunda akiwasilisha salamu zake
No comments: