Wafanyabiashara haramu ya Nzige watoweka wilayani Misungwi
Wasiliana na BMG kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma za Habari na Mangazo.
SOMA>>>Kampeni ya kutokomeza Ukatili Misungwi yahitimishwa kwa mafanikio
Mkuu wa wilaya Misungwi, Mhe. Juma Sweda akizungumza kwenye kilele cha kampeni ya kupambana na ukatili wa kijinsia wilayani Misungwi.
Kaimu Mkurugenzi Halmashauri ya Misungwi, Fredrick Nyoka akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa kampeni hiyo.
Kamanda wa Polisi mkoani Mwanza, ACP. Jonathan Shanna akiwasilisha salamu zake kwenye kilele cha kampeni hiyo.
Mkuu wa Wilaya Misungwi, Mhe. Juma Sweda akivishwa shuka la Sungusungu Kata ya Nhundulu wilayani Misungwi.
Mmoja wa Sungusungu wilayani Misungwi akitoa pongezi kwa Mkuu wa Wilaya hiyo, Mhe. Juma Sweda kwa juhudi zake za kupambana na ukatili wa kijinsia hususani mimba za utotoni na mauaji ya wanawake.
Mkuu wa Wilaya Misungwi, Mhe. Juma Sweda (kushoto), akimkabidhi Mwenyekiti wa Halmashauri ya Misungwi, Antony Bahebe cheti maalum kutoka shirika la KIVULINI kama ishara ya kutambua mchango wake katika mapambano dhidi ya ukatili wa kijinsia.
Mkuu wa Wilaya Misungwi, Mhe. Juma Sweda (kushoto), akimkabidhi Kaimu Mkurugenzi Halmashauri ya Misungwi, Fredrick Nyoka cheti maalum kutoka shirika la KIVULINI kama ishara ya kutambua mchango wake katika mapambano dhidi ya ukatili wa kijinsia.
Mkuu wa Wilaya Misungwi, Mhe. Juma Sweda (kushoto), akimkabidhi Afisa Maendeleo ya Jamii Misungwi cheti maalum kutoka shirika la KIVULINI kama ishara ya kutambua mchango wake katika mapambano dhidi ya ukatili wa kijinsia.
Burudani kwenye kilele cha kampeni hiyo
Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
Baadhi ya
wanawake maarufu kwa jina la Nzige waliokuwa wanafanya biashara haramu ya
kujiuza msimu wa mavuno katika wilaya ya Misungwi mkoani Mwanza, wametoweka
baada ya kukosa wateja (wanaume) kufuatia kampeni ya kutokomeza ukatili wa
kijinsia iliyoendeshwa wilayani humo.
Hayo
yalibainishwa juzi katika Kaya ya Nhundulu wilayani Misungwi wakati wa kufunga
kampeni hiyo iliyodumu kwa kipindi cha wiki nane ambayo imeendeshwa katika Kata
22 kati ya 27 za Wilayani hiyo, iliyolenga kutoa elimu ya kupambana na ukatili
wa kijinsia dhidi ya wanawake na watoto.
Mkurugenzi
shirika la KIVULINI, Yassin Ally alisema kampeni hiyo imewafikia wananchi
33,420 na kuleta matokeo chanya ikiwemo matumizi sahihi ya kipato msimu wa
mavuno ambapo sasa wanafamilia wanatumia vyema fedha hizo ikiwemo kujenga
nyumba bora, kununua magodoro ya kisasa badala ya yale ya nyasi maarufu kama
Dodoma Ngubalu huku kwa mara ya kwanza biashara haramu ya Nzige katika maeneo
mbalimbali kama Kidarajani ikitoweka kutokana na elimu iliyotolewa kupitia
midahalo ya wazi.
Akitoa
taarifa ya utekelezaji wa kampeni hiyo, Kaimu Mkurugenzi Halmashauri ya
Misungwi, Fredrick Nyoka alisema imesaidia kupunguza vitendo vya ukatili katika
jamii ikiwemo ubakaji, mimba za utotoni pamoja na matumizi mabaya ya fedha
msimu wa mavuno na kwamba wananchi wamejengewa utayari wa kuripoti vitendo
hivyo pindi vinapotokea.
Kufuatia
mafanikio hayo, Mkuu wa Wilaya Misungwi Mhe. Juma Sweda ambaye alikuwa mgeni
kwenye kilele cha kampeni hiyo, alitoa rai iwe endelevu ili kuzifikia Kata zote
wilayani humo huku akionya kuwashughulikia wale wote ambao hawataacha
kujihusisha na vitendo vya ukatili wa kijinsia katika jamii.
“…Nitakuwa
mkali kuliko pilipili, nitakuwa silali usiku na mchana kufuatilia wale ambao
wanaendelea na ukatili…wale wote wasiopenda kutenda haki wajue sasa watapambana
na mkono wa mwanaume wa shoka ambaye ni mimi katika mkoa wa Mwanza…”. Alionya
Kamanda wa Polisi mkoani Mwanza ACP. Jonathan Shanna.
Kampeni hiyo
ilizinduliwa Julai 04, 2018 na kuendeshwa na Halmashauri ya Wilaya Misungwi kwa
ushirikiano wa karibu na shirika la kutetea haki za wasichana/ watoto na
wanawake KIVULINI la Jijini Mwanza.
Tazama BMG Online Tv haoa chini
SOMA>>>Kampeni ya kutokomeza Ukatili Misungwi yahitimishwa kwa mafanikio
No comments: