Naibu Waziri Ulega aagiza uundaji wa Ushirika wa wavuvi Kanda ya Ziwa
Wasiliana na BMG kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma za Habari na Mangazo.
Judith Ferdinand, BMG
Naibu Waziri
wa Uvuvi na Mifugo, Abdallah Ulega amewaangiza Maofisa Uvuvi Kanda ya Ziwa kuhakikisha
wanaanzisha ushirika wa wavuvi wadogo wadogo katika mialo mbalimbali ikiwemo Kigangama wilaya ya Magu mkoani
Mwanza.
Ulega alitoa
agizo hilo jana alipotembelea Mwalo wa Kigangama uliopo Magu na Chuo cha Uvuvi
( FETA) kituo cha Gabimori wilayani Rorya wakati wa ziara yake katika mikoa ya
Mwanza na Mara.
"Nikirudi
hapa baada ya mwezi mmoja nataka nikute ushirika wa wavuvi wadogo wadogo
umeanzishwa katika mialo yote ikiwemo ya Kigangama Magu na Sota Rorya, hivyo
watendaji katika sekta ya uvuvi pamoja na wakuu wa wilaya mshirikiane kuhakikishe
mnasimamia suala hili kwani litawasaidia kuwa na sauti ya pamoja katika msimamo
wa bei pamoja na kutatua changamoto zao kama kukopeshwa mashine na nyavu za kisasa katika kuendeleza
kipato binafsi na taifa”. Alisema Ulega.
Alisema oparesheni
ya kudhibiti uvuvi haramu inaendelea hivyo wavuvi wafuate sheria, taratibu na
kanuni kwani kupitia kampeni hiyo wamegundua mambo mengi ikiwemo namna ambavyo
wavuvi wadogo wanavyo nyonywa na wachakataji wa samaki hususani katika bei
ambayo huacha maskini huku wenye viwanda wakinufaika zaidi.
"Mvuvi
anauza samaki kwa kilo moja shilingi 5,000 ambayo inamuacha masikini wakati
anatumia muda na gharama kubwa ya mfuta wakati wa kuvua na kumnufaisha
mchakataji ambaye anauza kichwa, ngozi, mnofu, mafuta, mifupa kwa bei kubwa
hususani bondo ambalo linauzwa kuanzia 100,000 hadi 600,000 kwa kilo hivyo
Serikali inaangalia namna ya kulikomboa kundi hilo ili liweze kunufaika”. Alisema.
Pia Ulega
alipata fursa ya kuteketeza zana haramu za kuvulia samaki ikiwemo nyavu, ndoano,
kokoro za samaki, dagaa pamoja na kamba.
Naye Afisa
Uvuvi Kanda ya Simiyu na Magu, Samson Mboje alisema kwa kipindi cha miezi
miwili kuanzia Agosti hadi Septemba mwaka huu wameweza kukamata zana za uvuvi haramu ikiwemo makokoro ya
samaki 112, ya dagaa 12, nyavu za samaki 78, kamba za kokoro 52,500 ambavyo Naibu
Waziri ameviteketeza na kwamba ndoano 5,500 zinaombewa kibali mahakamani ili
kuziyeyusha katika kiwanda cha Nyakato Steel kwani ni chuma.
Naye Katibu
wa BMU mwalo wa Kigangama, John Masato alisema wanakabiliwa na wizi wa zana za
uvuvi ziwani pamoja na kuuzwa kwa bei ghali na kushuka kwa bei ya mazao ya
samaki.
Aidha
Mwenyeikti wa Halmashauri ya Wilaya ya Rorya, Albert Machiwa aliiomba Serikali
kuongeza ulinzi kwa kufanya doria ziwani hususani katika maeneo yaliyopakana na
nchi jirani za Kenya na Uganda ambapo askari wao pamoja na watanzia wachache
wasio waadilifu wamekuwa wakiwapiga wavuvi.
No comments: