LIVE STREAM ADS

Header Ads

DC Misungwi aingilia kati mgogoro wa wachimbaji wadogo wa madini

Wasiliana na BMG kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma ya Habari na Mangazo.

Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
Mkuu wa Wilaya Misungwi mkoani Mwanza, Mhe. Juma Sweda ameagiza kupitiwa upya mkataba baina ya kikundi cha wachimbaji wadogo wa dhahabu Nyabayombe kilichopo katika Kijiji cha Lubili pamoja na Mwekezaji Seif Mahumbi baada ya kuibuka mgogoro wa kimaslahi.

Mhe. Sweda aliyetembelea machimbo hayo wiki iliyopita, alisema hatambui mkataba huo ambao unampa mwekezaji haki ya asilimia 70 ya mauzo ya dhahabu baada ya kusababisha mvutano wa kimaslahi baina ya kikundi hicho na ushirika wa wachimbaji wadogo wa dhahabu wa Misungwi Mining Corperative Society Limited (MIMICOSO) uliokuwa na makubaliano ya uchimbaji pamoja na kikundi hicho cha Nyabayombe.

Ilielezwa kwamba chimbuko la mgogoro huo ni baada ya kikundi cha Nyabayombe kinachomiliki leseni 16 za uchimbaji dhahabu kuzuia ushirika wa MIMICOSO kuendelea na shughuli zake kulingana na makubaliano yaliyokuwepo baada ya kuingia ubia mwingine na mwekezaji Mahumbi.

Baadhi ya wanachama wa kikundi hicho cha Nyabayombe waliwatupia lawama viongozi wao kwa kusababisha mgogoro huo baada ya kuingia makubaliano na mwekezaji ambayo wao hawayatambui huku wakimshukuru DC Sweda kwa kwa kutotambua mkataba huo na kuwaruhusu kuendelea na shughuli zao.

Mwakilishi wa Afisa Madini Mkazi mkoa Mwanza, Ndembi Nkingwa aliwataka wamiliki wa leseni za uchimbaji madini kuzingatia sheria wakati wa kuingia ubia na wawekezaji ili kuondokana na migogoro isiyo ya lazima. 
Tazama BMG Online TV hapa chini

No comments:

Powered by Blogger.