Serikali yasisitiza msimamo wa kuufunga mgodi wa kokoto wilayani Bagamoyo
Wasiliana na BMG kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma za Habari na Matangazo.
Naibu Waziri
wa Madini, Mwl. Doto Mashaka Biteko amefika katika machimbo (mgodi) ya kokoto
Lugoba, Bagamoyo mkoani Pwani na kuridhishwa na utendaji kazi katika machimbo
hayo.
Mwl. Biteko
ametoa pongezi kwa kampuni ya Yaate Investment kwa kushirikiana na kampuni ya
Yapi Merkezi kwa uwekezaji mzuri unaozingatia sheria ya madini.
Akiwa katika
machimbo hayo, ametoa muda usiozidi siku tano hadi jumatatu wiki ijayo kwa Bw.
Akram Aziz ambaye ametelekeza mitambo/ vifaa yake ya uchimbaji kokoto katika
eneo hilo vinginevyo hatua kali zitachukuliwa dhidi yake kwani ni kosa kisheria
kutelekeza mitambo hiyo kwenye eneo la leseni ya uchimbaji lisilo lake.
Ifahamike
kwamba malighafi za ujenzi wa reli ya kisasa (Standard Gauge Railway) zinatoka
katika mgodi huo.
Katika hatua
nyingine, Mwl. Biteko ametoa msimamo wa serikali wa kuendelea kuufunga mgodi wa
kokoto unaomilikiwa na kampuni ya Lugoba Tan-Turk Stone Quarry hadi utakawalipa
fidia wakazi wanaozunguka mgodi huo ili wapishe shughuli kuendelea.
Uongozi wa
mgodi huo kupitia kwa Mkurugenzi wake, Raci Omary umeomba kupewa muda hadi
mwezi Disemba mwaka huu ili kutoa fidia kwa wakazi hao.
Sehemu ya mchanga na kokoto katika mgodi wa kokoto Yaate Investment
Sehemu ya mchanga na kokoto katika mgodi wa kokoto Yaate Investment
Naibu Waziri wa Madini, Mwl. Doto Biteko akikagua mgodi wa Lugoba Tan-Turk Stone Quarry ambao umefungiwa.
Naibu Waziri wa Madini, Mwl. Doto Biteko akikagua eneo la upasuaji kokoto katika mgodi wa Lugoba Tan-Turk Stone Quarry
Sehemu ya mitambo iliyotekelezwa katika eneo la mgodi wa upasuaji kokoto wa Yaate Investment
No comments: