LIVE STREAM ADS

Header Ads

BAKWATA mkoani Geita kuanza utekelezaji wa miradi mikubwa

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa Binagi Media Group. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com
Na Joel Maduka, Geita
Baraza Kuu la Waislamu (BAKWATA) mkoani Geita linatarajia kuanza ujenzi wa jengo la ghorofa nne litakalogharimu zaidi ya shilingi biloni tatu ambapo litakuwa na Msikiti, maduka zaidi ya 100, kumbi za mikutani pamoja na vyumba vya kulala wageni.

Mwenyekiti wa Baraza hilo, Alhaji Said Karidushi amesema kuanzishwa kwa miradi hiyo kutafungua mwanya mkubwa wa kuwasaidia watu mbalimbali hususani katika sekta ya elimu na afya.

Karidushi amesema pia Baraza hilo linatarajia kujenga Chuo cha Mafunzo kitakachowahudumia wanajamii kutoka dini zote.

Naye Sheikh Mkuu wa Mkoa Geita, Alhad  Yusuf Kabaju amesema miradi hiyo inatarajiwa kuanza mwaka huu na kukamilika kwa wakati kwani lengo ni kuhakikisha BAKWATA inakua kiuchumi na kutimiza malengo yake.

No comments:

Powered by Blogger.