LIVE STREAM ADS

Header Ads

Benki ya CRDB yakabidhi Milioni 20 katika Hospitali ya Sekou Toure Jijini Mwanza

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa Binagi Media Group. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com
Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
Benki ya CRDB imekabidhi hundi ya shilingi Milioni 20 katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Mwanza, Sekou Toure ili kusaidia ukarabati na ununuzi wa vifaa tiba katika wodi ya upasuaji (Theatre) ya akina mama katika Hospitali hiyo.

Akizungumza kwenye hafla fupi ya kukabidhi hundi hiyo, Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya CRDB, Dkt. Joseph Witts alisema benki hiyo ni mdau mkubwa katika kuboresha huduma za afya hapa nchini ambapo imekuwa ikitoa asilimia moja ya faida yake kwa ajili ya kuwasaidia wananchi.

Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Mwanza, Dkt. Bahati Msaki aliishukru Benki ya CRDB kwa mchango huo na kwamba utasaidia kuondoa changamoto ya utoaji huduma za afya kwa akina mama.

Mbali na hundi hiyo, pia Benki ya CRDB ilikabidhi luninga (TV) tatu za kisasa katika Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Ziwa, Bugando  ili kutoa huduma kwa wananchi na wagonjwa wanaofika katika hospitali hiyo.
Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya CRDB, Dkt. Joseph Witts akizungumza kwenye hafla hilo.
Baadhi ya watumishi wa Benki ya CRDB.
Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella akipokea hundi ya shilingi Milioni 20 kutoka Benki ya CRDB. Makabidhiano hayo yameshuhudiwa na Katibu Tawala mkoani Mwanza, Dkt. Christopher Kadio, Mwenyekiti wa Bodi Hospitali ya Sekour Toure, Christopher Gachuma, Mganga Mkuu Hospitali hiyo, Dkt. Thomas Rotachunzibwa pamoja na watumishi wa Hospitali hiyo.
Makabidhiano hayo yakiendelea
Tazama BMG Online TV hapa chini

No comments:

Powered by Blogger.