Mbunge wa Kwimba awekeza zaidi ya bilioni moja kwenye kuku
Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa Binagi Media Group. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com
Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
Mbunge wa
Jimbo la Kwimba mkoani Mwanza, Shanif Mansoor (CCM) ametumia zaidi ya shilingi
bilioni moja kuwekeza katika shamba la kisasa la ufugaji wa kuku wa mayai
katika eneo la Nyanguge wilayani Mwanza.
Mansoor
ambaye ni Mkurugenzi wa shamba hilo liitwalo SMJ Poultry Egg Farm anafafanua
kuhusiana na uwekezaji huo mkubwa mbele ya Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella
aliyemtembelea, Januari 11, 2019.
Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella (kulia), akipata ufafanuzi kutoka kwa Mbunge wa Jimbo la Kwimba, Shanif Mansoor (wa pili kulia) kuhusiana na mradi wake wa ufugaji kuku wa mayai.
Mashine za kuandaa chakula cha kuku.
Mbunge wa Jimbo la Kwimba mkoani Mwanza, Shanif Mansoor (mwenye nguo nyekundu) akitoa ufafanuzi kuhusu mradi wake wa ufugaji wa kuku kwa Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella (mwenye kofia), aliyeambatana pia na Mkurugenzi Halmashauri ya Magu, Lutengano Mwalwiba (kulia), Mkuu wa Wilaya Magu Dkt. Philemon Sengati (kushoto) pamoja na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya Magu, Hilal Elisha (wa pili kushoto).
Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella akiwa kwenye picha ya pamoja na wafanyakazi wa mradi wa kuku SMJ Poultry Egg Farm.
Tazama BMG Online TV hapa chini
No comments: