Waliomsaidia mama kujifungua mapacha wanne wasimlia
Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa Binagi Media Group. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com
Wauguzi
katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Mwanza Sekou Toure ambao walimsaidia mama Jenipher
John (23) mkazi wa Ibanda Manispaa ya Ilemela kujifungua mapacha wanne Januari 09,
2019 majira ya saa saba mchana wameeleza mwanzo mwisho shughuli hiyo ilivyokuwa.
Mama huyo
ambaye mimba yake ya kwanza pia ilikuwa ya mapacha wanne japo Aprili 2018 iliharibika ikiwa
na miezi sita, anaiomba serikali kumsaidia kulea watoto hao kwani peke yake
hawezi kwa kuwa hana shughuli ya kumuingizia kipato huku mme wake anayefanya
kazi ya kuendesha pikipiki (bodaboda) akiwa na uchumi wa kawaida.
No comments: