LIVE STREAM ADS

Header Ads

Serikali yaanza kutoa mafunzo kwa wachimbaji wadogo wa madini

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa Binagi Media Group. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com
Naibu Waziri wa Madini, Doto Biteko (pichani) amefungua mafunzo ya siku mbili kuanzia leo Januari 04, 2018 kwa wachimbaji wadogo wa madini/ dhahabu yaliyofanyika katika Kijiji cha Byatika Kata ya Buhemba Wilaya ya Butiama mkoani Mara.

Mafunzo kama hayo yanaendelea kwa nyakati tofauti katika maeneo mbalimbali nchini ambapo juzi Januari 02, 2018 Biteko alifungua mafunzo kwa wachimbaji wadogo wa dhahabu/ madini katika Wilaya ya Bukombe mkoani Geita.

Mafunzo hayo yanatolewa na Serikali kupitia taasisi zake ikiwemo Tume ya Madini pamoja na Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini (GST) ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa ombi la wachimbaji wadogo wa madini hapa nchini ambao waliomba kupatiwa mafunzo ili kufanya shughuli zao kwa weledi bila kubahatisha.
Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
Afisa Madini mkoani Mara, Nyaisara Mgaya akifafanua jambo wakati wa mafunzo hayo.
Godson Kamihanda kutoka Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini hapa nchini (GST) akizungumza wakati wa mafunzo hayo ambapo katika mafunzo hayo taasisi hiyo itatoa taarifa ya utafiti wa madini hapa nchi ili uwasaidie wachimbaji kufanya kazi zao bila kubahatisha.
Wachimbaji wadogo wa dhahabu wakifuatilia kwa umakini mafunzo hayo.
Naibu Waziri wa Madini, Doto Biteko (aliyekaa kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na viongozi mbalimbali wa serikali pamoja na wachimbaji wadogo wa dhahabu katika wilaya ya Butiama mkoani Mara.
Naibu Waziri wa Madini, Doto Biteko (aliyekaa kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na viongozi mbalimbali wa serikali pamoja na wachimbaji wadogo wa dhahabu katika wilaya ya Butiama mkoani Mara.
Naibu Waziri wa Madini, Doto Biteko (aliyekaa kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na viongozi mbalimbali wa serikali pamoja na wachimbaji wadogo wa dhahabu katika wilaya ya Butiama mkoani Mara.
Naibu Waziri wa Madini, Doto Biteko (aliyekaa kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na viongozi mbalimbali wa serikali pamoja na wachimbaji wadogo wa dhahabu katika wilaya ya Butiama mkoani Mara.
Awali Naibu Waziri wa Madini, Doto Biteko alipita katika ofisi ya Mkuu wa Wilaya Butiama, Anna Rose Nyambi (pichani) na kupokea taarifa ya hali ya uchimbaji madini katika wilaya hiyo.
Tazama BMG Online TV hapa chini

No comments:

Powered by Blogger.