Mkuu wa Wilaya Tunduru aeleza manufaa ya uanzishwaji masoko ya madini
Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa Binagi Media Group. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com
Mkuu wa Wilaya Tunduru mkoani Ruvuma, Juma Homera akizungumza na BMG kando ya warsha kwa viongozi na wadau wa madini kuhusu mswada wa kanuni za uanzishwaji masoko ya madini nchini inayofanyika jijini Mwanza.
Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
Wizara ya
Madini kwa kushirikiana na taasisi ya “UONGOZI Institute” imeandaa warsha kwa
viongozi na wadau wa madini inayolenga kujadili maudhui ya kanuni mpya za uanzishwaji
masoko ya madini hapa nchini kama alivyoagiza Rais Dkt. John Pombe Magufuli
hivi karibuni Jijini Dar es salaam.
Warsha hiyo
ya siku mbili ilifunguliwa jana jijini Mwanza na Waziri wa Madini, Doto Biteko
ikiwashirikisha Maafisa Madini, Makatibu Tawala, Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi
wa Halmashauri pamoja na viongozi wa wachimbaji wadogo wa madini kutoka mikoa
ya Dodoma, Arusha, Geita, Shinyanga, Mara, Manyara, Njombe, Kagera, Tabora,
Singida, Mbeya, Morogoro na Ruvuma.
Mkuu wa
Wilaya Tunduru mkoani Ruvuma, Juma Homera amezungumza na BMG Online TV na
kubainisha mtazamo wake kuhusiana na kanuni hizo za uanzishwaji masoko ya
madini nchini ambazo zinaelezwa kwamba zitapunguza utoroshwaji wa madini, kero
na malalamiko ya wachimbaji na wafanyabiashara wa madini ikiwemo mlolongo wa
kodi na tozo mbalimbali.
Tazama BMG Online TV hapa chini
No comments: