LIVE STREAM ADS

Header Ads

Wanawake migodini walia kubaguliwa wakati wa hedhi "wanasema tunazuia dhahabu"

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa Binagi Media Group. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com

Na Joel Maduka, Geita
Suala la mfumo dume bado limeendelea kutajwa kuwa kisababishi kikubwa kwa wanawake kubaguliwa katika maeneo ya migodini na hivyo kusababisha wengi wao kushindwa kujikwamua kiuchumi.

Hayo yameelezwa kwenye mkutano wa shirika lisilo la kiserikali la Biashara na Haki za Binadamu, kwa kushirikiana na wanawake wachimbaji wa madini mkoani Geita.

Baadhi ya wanawake wachimbaji wa madini ya dhahabu mkoani humo wanawasema, wamekuwa wakizuiliwa kufika kwenye mashimo ya kuchimba dhahabu wanapokuwa kwenye mzunguko wa hedhi kwa madai kwamba wanaweza kusababisha dhahabu kutopatikana. 

Mwenyekiti wa  chama  cha  wanawake wachimbaji dhahabu koani Geita (GEWOMA), Asia Hussein anasema kukosekana kwa elimu kwa wanawake wengi wa maeneo ya migodi ni chanzo kinachosababisha mfumo dume kuendelea kuwepo maeneo ya migodini.

Naye Theresia Sawale ambaye ni mratibu wa mradi wa ushirikishaji jinsia katika masula ya madini kutoka shirika la Biashara na Haki za Binadamu anasema shirika hilo limeanza kutoa elimu kwa wanaume maeneo mbalimbali ikiwemo migodini ili kutambua thamani ya mwanamke katika kujitafutia kipato hususani maeneo ya migodini. 
Tazama BMG Online TV hapa chini

No comments:

Powered by Blogger.