LIVE STREAM ADS

Header Ads

Mwanaharakati Flora Lauwo awasili Jijini Mwanza na tuzo zake

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa Binagi Media Group. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com

Mkurugenzi wa Taasisi ya Nitetee Foundation ya Jijini Mwanza, Flora Lauwo asubuhi ya leo Machi 23, 2019 amepokelewa kwa shangwe katika uwanja wa ndege wa Mwanza akitokea nchini Oman alikokuwa amealikwa kutokana na mchango wake mkubwa wa kusaidia watu mbalimbali wenye uhitaji katika jamii kupitia taasisi yake.

Mwezi mmoja uliopita, Lauwo kupitia Ubalozi wa Tanzania alialikwa nchini Oman ambapo Machi 08, 2019 kwenye Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani alipatiwa tuzo mbili za kama ishara ya kutambua mchango wake wa kuwasaidia wenye uhitaji katika jamii. 

Pia kwenye maadhimisho hayo (Siku ya Wanawake Duniani 2019), Lauwo alipewa tuzo kupitia tamasha la Binti Filamu lililofanyika Jijini Mwanza na hivyo kufanya idadi ya tuzo alizopokea mwaka huu kuwa tatu. Lauwo pia amewahi kushinda tuzo ya Malikia wa Nguvu inayotolewa na Clouds Media Group.
Tazama BMG Online TV hapa chini

Shuhudia Miss Mwanza akitangazwa
#PamojaDaimaBMG

No comments:

Powered by Blogger.